Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AJALI YA NDEGE YAUA 50 URUSI.

Ndege ya abiria imeanguka katika uwanja wa ndege katika mji wa Kazan, nchini Urusi na kuua watu wote 50 waliokuwa katika ndege hiyo.Ndege hiyo aina ya Boeing 737 iliruka kutoka mji wa Moscow na ilikuwa ikijaribu kutua lakini ikawaka moto saa moja usiku kwa saa za huko.

Wizara ya matukio ya dharura imesema kulikuwa na abiria 44 na wafanyakazi sita wa ndege hiyo ya shirika la Tatarstan Airlines.

Wachunguzi wanajaribu kuona kama kulikuwa na makosa ya kiufundi au huenda ya kibinadamu yaliyosababisha ajali hiyo.

Afisa wa kamati ya uchunguzi Vladimir Markin ameiambia Televisheni moja nchini Urusi, Rossiya 24 TV, kwamba wataalam wanachunguza kubaini kama ajali hiyo imesababishwa na matumizi ya mafuta mabaya, au hali mbaya ya hewa.

Mvua ilikuwa ikinyesha katika mji wa Kazan wakati ndege hiyo ilipoanguka.

Kwa mujibu wa orodha rasmi ya wasafiri wa ndege hiyo, miongoni mwa waliokufa ni Irek Minnikhanov, mtoto wa kiume wa rais wa Jamhuri ya Tatarstan,nchini Urusi.


Aleksander Antonov, ambaye aliongoza Idara ya Usalama ya Shirikisho la Urusi, ni miongoni mwa abairia wa ndege iliyoanguka.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, imethibitisha kuwa raia mmoja wa Uingereza amekufa katika ajali hiyo.

Miongoni mwa waliokufa wamo watoto wawili.

Rais Vladimir Putin wa Urusi ametuma salaama zake za rambirambi kwa ndugu na jamaa wa waathirika.

Tume ya serikali imeundwa kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.

Taarifa zinasema, rubani wa ndege hiyo Rustem Salikhov mwenye umri wa miaka 47, alijaribu mara kadhaa kutua kabla ya kuanguka kwa ndege hiyo.

Shirika la habari la Urusi limeripoti kuwa wafanyakazi walisema hawakuwa tayari kutua kwa sababu ya matatizo ya kiufundi.

Mwandishi mmoja wa habari ambaye alisafiria ndege hiyo mapema Jumapili kabla ya safari iliyotokea ajali, kutoka Kazan kwenda Moscow ameiambia televisheni moja nchini Urusi kwamba kulikuwa na mtetemo mkubwa wakati ndege hiyo ikitua mjini Moscow.

"Tulipokuwa tukitua haikujulikana kama kulikuwa na upepo mkali, japokuwa mjini Moscow, hali ya hewa ilikuwa nzuri au kulikuwa na tatizo la kiufundi au ndege yenyewe," amesema Lenara Kashafutdinova.

"Tulisukwasukwa huku na kule, ndege ilitua. Mtu aliyekuwa amekaa karibu nami alikuwa mweupe kama shuka kutokana woga uliompata."

Ndege hiyo imekuwa ikitoa huduma tangu mwaka 1990.

Uwanja wa ndege wa Kazan - mji mkuu wa Tatarstan - umefungwa tangu kutokea jali hiyo na hautarajiwi kufunguliwa hadi Jumatatu mchana.

Mji wa Kazan upo kilomita 720 mashariki mwa Moscow.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe