Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NGASA AITANGAZIA VITA SIMBA, AAPA KUILIZA OKTOBA 20

Winga Mrisho Ngasa (Pichani) wa Yanga amesema ataendelea kucheza kwa kujituma zaidi ili kukisaidia kikosi chake hicho kipya kufikia malengo na kuweka wazi kwamba amejipanga kuifanyia 'kitu mbaya' Simba katika mechi yao ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara itakayochezwa Oktoba 20.


Ngasa alilazimika kuwalipa Simba Sh. milioni 45 (Sh. milioni 30 alizochukua ili kusaini kuichezea klabu hiyo na Sh. milioni 15 za fidia), jambo lililofanya licha ya kuitumikia bado "imekula kwake" na Simba ndiyo iliyonufaika.

Wakati akiendelea kuuguza machungu ya kulipa mamilioni hayo, Ngasa anataka kufidia maumivu yake dhidi ya Simba kwa kutumia mpira uwanjani.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mechi yao ya juzi waliyoshinda 1-0 dhidi ya 'maafande' wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana, Ngasa alisema kuwa ana deni kwa mashabiki wa Yanga, hasa baada ya kukosa mechi sita za timu yao ikiwamo ya Ngao ya Hisani walioshinda 1-0 dhidi ya Azam na tano za ligi kuu baada ya kufungiwa na Shirikisho la Soka (TFF).

Ngasa, ambaye juzi alitoka kifungoni na kutoa pasi ya mwisho ya goli pekee la mechi lililofungwa na mshambuliaji Mganda Hamis Kiiza, alisema anaisubiri kwa hamu mechi yao dhidi ya Simba ili 'kumaliza hasira zake' za zilizotokana na kuamuliwa kulipa mamilioni ya fedha.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF ilimfungia mechi sita mzaliwa huyo wa jiji la Mwanza na kumtaka alipe Sh. milioni 45 baada ya kubaini kuwa aliingia mkataba na Simba kwa ajili ya kuitumikia il-hali bado alikuwa na mkataba na Azam.

Hata hivyo, hukumu hiyo ililalamikiwa kwamba ilitolewa kisiasa kwa maelezo kwamba Simba pia ilipaswa kuadhibiwa kwa kuhusika katika jambo hilo, kwa kumsainisha mkataba mchezaji ambaye ilitambua kuwa alikuwa bado ana mkataba na timu nyingine wakati walipomchukua kwa mkopo wa mwaka mmoja kutoka Azam.

Baada ya kutoa pasi ya goli la ushindi juzi, Ngasa alikwenda jirani na jukwaa la Simba na kuanza kuwapungia mikono 'Wanamsimbazi', ishara ambayo alisema kuwa inamaanisha ameanza kazi na wajiandae kwa kipigo Oktoba 20.

"Nina deni kubwa kwa mashabiki wa Yanga, namshukuru Mungu nimemaliza adhabu na leo (juzi) nimetoa pasi ya goli... Simba wajiandae tutakapokutana nao tutawaonyesha kazi," alisema Ngasa ambaye katika mechi ya juzi alicheza vizuri licha ya kuwa nje ya uwanja tangu kuanza kwa ligi hiyo inayodhaminiwa na Vodacom Agosti 24.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa