Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIPUTE ULAYA FILIMBI YAPULIZWA, MESSI NJE WIKI TATU

Steaua Bucharest  v Chelsea

Kundi E: Jumanne Saa 3.45 usiku
Steaua imepaa kileleni kwa pionti tatu zaidi katika Ligi Kuu ya Romania, baada ya kuilaza Poli Timisoara mabao 3-0, ambayo yalitiwa kimiani na Federico Piovaccari, Nicolae Stanciu na Adrian Popa.
Arsenal v Napoli

Kundi F: Jumanne Saa 3.45 usiku
Mabao mawili ya Goran Pandev yameipa Napoli pointi tatu dhidi ya Genoa na kupaa kileleni mwa Ligi Kuu Italia, Serie A. Wanalingana kwa pointi na Juventus, 16 kila timu baada ya mechi sita, lakini wanashika usukani kwa wastani wao mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Kundi H: Jumanne Saa 3.45 usiku

Lionel Messi ataikosa mechi hiyo na kuwa nje kwa wiki tatu nyingine, baada ya kuumia nyama za mguu wake wa kulia.

Mwanasoka huyo bora wa dunia alitolewa wakati timu yake ikhinda 2-0 dhidi ya Almeria Jumamosi muda mfupi tu baada ya kufunga bao la kwanza dakika ya 21, ambalo lilikuwa bao lake la nane msimu huu.

Kundi D: Jumatano Saa 3.45 usiku

Thomas Muller alifunga bao pekee katika mchezo mgumu wakati Bayern Munich ikiifunga Wolfsburg 1-0 na kuendelea kukabana koo na Dortmund kileleni mwa Bundesliga. Wana pointi 19 baada ya mechi saba bila kufungwa hata moja.

Kundi A: Jumatano Saa 3.45 usiku

Shakhtar imepanda hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Ukraine, baada ya Eduardo kuwafungia bao la kusawazisha dakika za lala salama dhidi ya mahasimu wao wa Jiji, Metalurh.

Walikuwa wamekwishalala 2-0 lakini walirudisha moja kupitia kwa Alex Teixeira dakika ya 54 na wakajipatia pointi moja, baada ya mshambuliaji wa zamani wa Arsenal kusawazisha zikiwa zimesalia dakika nane.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa