Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIPSANG AVUNJA REKODI YA BERLIN MARATHON

Mkenya Wilson Kipsang amevunja rekodi ya dunia ya mbio za Marathon kwa kupunguza sekunde 15 aliposhinda mbio za Berlin mapema jumapili.


Mkimbiaji huyo mwenye umri wa miaka 31 aliandikisha mda wa saa mbili dakika tatu na sekunde 23 kuondoa rekodi ya zamani iliyowekwa na Mkenya mwenzake Patrick Makau miaka miwili iliyopita.

Rekodi hiyo iliwekwa katika mji mkuu wa Ujerumani ambako Makau alikimbia kwa mda wa saa 2:dakika 03:na sekunde 38.
Wilson Kipsang

Kipsang katika mitaa ya Berlin

Wakenya wengine walioshiriki mbio a Berlin Eliud Kipchoge alimaliza katika mda wa saa 2:04:05) huku Geoffrey Kipsang akiweka mda wa saa 2:06:26 katika nafasi ya tatu.

Makau hakushiriki mbio hizi baada ya kujiondoa wiki mbili zilizopita kutokana na kuuguza jeraha la goti.

Wilson alifanya mazowezi akiwa na nia ya kuvunja rekodi ya Berlin na moja kwa moja alianza mbio za leo kwa kudhibiri uongozi katika hatua ya kilomita 10 za mwisho, akiwaacha wenzake walioonekana kuishiwa na pumzi ya kumkimbiza.

Baada ya mbio hizi Kipsanga alisema," Nimefurahi sana kwa ushindi huu na kwa kuvunja rekodi,"

"nilivutiwa mno na Paul Tergat wakati akikimbia na kuvunja rekodi hii miaka kumi iliyopita katika mashindano haya haya.

Ushindi wa Kipsang unampa jumla ya ushindi wa saba tangu aanze kushiriki mashindano ya marathon mjini Paris,Ufaransa miaka mitatu iliyopita.

Itakumbukwa kuwa Kipsang alishinda mbio za marathon za London mwaka jana na kwenye michezo ya Olimpiki alimaliza wa tatu na kujishindia medali ya fedha mjini London.

Ushindi wa mbio hizi za Berlin ni wa kwanza mwaka huu. Licha ya mbio za London kua mojapo ya mbio muhimu duniani na kwake aliweza kumaliza wa tano mapema mwezi Aprili mwaka huu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa