CRISTIANO RONALDO ADHIHIRISHA MSHAHARA WAKE, APIGA MBILI REAL IKIUA

PAMOJA na kumkosa mchezaji ghali duniani, Gareth Bale, lakini mchezaji anayeliwa mshahara mkubwa zaidi duniani, Cristiano Ronaldo alitosha kuipa pointi tatu Real Madrid usiku huu, baada ya kufunga mabao yote katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Elche.


Bale atarejea katika mechi ya nyumbani na Atletico Madrid Jumamosi wakati leo Ronaldo, ameendelea kuiweka Real karibu vinara wa La Liga.
Ronaldo alifunga mabnao hayo katika dakika za 51 na dakika ya sita ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90, wakati bao la kufutia machozi la Elche lilifungwa na Richmond Boakye dakika ya pili ya muda wa nyongeza baada ya kutimua dakika 90.

Kikosi cha Elche kilikuwa: Elche: Manu Herrera; Damián, Botía, Lombán, Albácar; Rubén Pérez, Carlos Sánchez; Stevanovic, Coro, Fidel na Boakye.

Real Madrid: Diego López, Pepe, Ramos, Coentrão, Khedira, Ronaldo, Benzema, Arbeloa, Modric, Di María na Isco.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI