Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AMISI TAMBWE AZITISHA YANGA, MBEYA CITY

Baada ya kufunga mabao manne katika ushindi wa 6-0 Simba iliyoupata dhidi ya Mgambo JKT juzi, mshambuliaji wa timu hiyo, Mrundi Amisi Tambwe (Pichani) ametamba kuendelea kufumania nyavu Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu, ikiwano mechi dhidi ya Yanga.


Tambwe aliyetua Simba msimu huu baada ya kuipa Klabu ya Vital'O ubingwa wa Ligi Kuu Burundi  pamoja na Kombe la Kagame, alisema kinachoendelea sasa ni kazi ya kucheka na nyavu tu.

Akizungumza katika mahojiano maalum baada ya kumalizika mechi dhidi ya Mgambo JKT iliyopigwa Uwanja wa Taifa juzi, Tambwe alisema ilimchukua muda kabla ya kuufahamu vema mfumo wa timu hiyo, lakini sasa haumsumbui tena.

Alisema licha ya kabla ya juzi kocha Abdallah Kibadeni kumchezesha kwa dakika zote 180 wakati wakishinda 1-0 dhidi ya Oljoro JKT Agosti 28, mwaka huu jijini Arusha, na baadaye kuwamo katika kikosi kilichoibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, alikuwa hajaushika vema mfumo wa timu hiyo.

Tambwe ambaye kwa sasa anaongoza kwa ufungaji katika ligi hiyo baada ya kufumania nyavu mara nne, huku akifuatiwa na Jerry Tegete wa Yanga na kiungo wa Simba, Haruna Chanongo wenye mabao matatu kila mmoja, hakucheza mechi ya ufunguzi dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora.

Katika mechi hiyo ya ufunguzi iliyopigwa Uwanja Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora na kumalizika kwa sare ya 2-2, Tambwe na Mrundi mwenzake, Gilbert Kaze walizuiwa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) kwa kutokana na kukosa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC).

"Nilikuwa sijazoea mfumo wa klabu yangu (Simba) na ligi ya Tanzania ambayo ni ngumu kuzidi ya kwetu (Burundi). Sasa nimeshazoeana na wachezaji wenzangu ndiyo maana nimefunga mabao haya," alisema Tambwe.

"Nafanya mazoezi kwa kujituma, natumai nitafanya vizuri zaidi katika mechi zinazofuata. Licha ya kuibuka na ushindi mnono, Mgambo ni timu nzuri. Nitaendelea kufanya kazi kwa kujituma zaidi ili pia nifunge katika mechi zinazofuata kwani kwa kufanya hivyo nitawapa raha mashabiki wangu na klabu ya Simba."

Msimu uliopita katika Ligi Kuu ya Burundi, Tambwe aliibuka mfungaji bora baada ya kufunga mabao 21 katika mechi 18, na baadaye kufanya hivyo tena kwa kufumania nyavu mara sita kwenye michuano ya Kombe la Kagame iliyofanyika mjini Darfur, Sudan na Vital'O kutwaa ubingwa.

Mrundi huyo anatajwa kuwa mrithi sahihi wa Mganda Emmanuel Okwi ambaye aliuzwa Klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia msimu uliopita, jambo ambalo lilichangia Simba kupoteza ubingwa kwa mahasimu wao wa jadi, Yanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa