Ruka hadi kwenye maudhui makuu

VALENCIA YAMPANDIA DAU CHICHARITO, MAN U WAINGIA MCHECHETO

KLABU ya Valencia inamtaka mshambuliaji wa Manchester United, Javier Hernandez maarufu kama Chicharito (Pichani) kwa mkopo.


Klabu hiyo ya Hispania imeandaa orodha fupi kusaka mchezaji wa kuziba pengo la Roberto Soldado ambaye anakaribia kujiunga na Tottenham, lakini pia anatakiwa na Liverpool.
Valencia imeweka bajeti maalum na hiyo inahusisha pia mshambuliaji kinda wa Manchester City,John Guidetti.
Target: Valencia want to bring Javier Hernandez to Spain to replace their departing striker
Anatakiwa: Valencia inamtaka Javier Hernandez ahamie Hispania kuziba pengo la mshambuliaji wake anayetaka kuondoka
Incoming: Roberto Soldado is a target for Tottenham and Liverpool
Anaondoka: Roberto Soldado anatakiwa na Tottenham na Liverpool

Pamoja na hayo, wanaamini wanaweza kumpata Hernandez kwa sababu kwa sasa hana namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha Mashetani Wekundu.
Mshambuliaji huyo wa Mexico amekuwa hatumiki sana kwa miezi 18 iliyopita, kufuatia kuwasili kwa Robin van Persie. Pia amekuwa akijadiliwa na Atletico Madrid na Juventus katika miezi ya karibuni, lakini amerudia kusema anataka kubaki Old Trafford.
Kocha David Moyes ni shabiki mkubwa wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 na haitakuwa rahisi kumruhusu kuondoka, hususan kutokana na kwamba United bado haijasajili mchezaji mwenye jina kubwa inamyemtaka.
Mustakabali wa Wayne Rooney pia unachangia, United inapambana kumzuia mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England kumzuia kuhamia kwa wapinzani Chelsea na Arsenal.
Big fan: David Moyes likes Hernandez and will be reluctant to let him leave
Shabiki mkubwa: David Moyes anampenda Hernandez na haitakuwa rahisi kumruhusu kuondoka

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa