Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA YAMALIZA KUSAJILI, YABARIKI KUMTOSA KIIZA

Klabu ya Yanga imesema imefunga usajili wa wachezaji wazawa, siku mbili baada ya kumchukua mlinda mlango Deogratias Munishi 'Dida' kutoka timu ya Azam.

Akizungumza  jana, Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga Abdallah bin Kleb alisema wamefanyia kazi mapendekezo ya kocha Ernest Brandts juu ya wachezaji wazawa aliokuwa akitaka kuwaongeza kwenye kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao.

Bin Kleb alisema usajili wa mlinda mlango huyo ambaye amewahi kuzichezea Simba kabla ya kuhamia Azam, ulipendekezwa na Brandts baada ya kuachana na mpango wa kumsajili kipa wa zamani Mghana, Yaw Berko.

"Usajili wetu umefanyika baada ya mapendekezo ya kocha wetu... ni yeye aliyetaka tumsajili Dida na tumefanya hivyo," alisema Bin Kleb.

Aidha, alisema baada ya Dida hakuna nafasi ya mchezaji wa ndani kwa kuwa tayari wamemaliza kufanyia kazi mapendekezo ya Brandts kwa upande wa wazawa.
Alisema wataongeza mchezaji mwingine mmoja kutoka nje ya nchi bila ya kumtaja mchezaji huyo wala nchi anayotokea.

"Siwezi kukuambia kitu ambacho hatujakikamilisha," alisema Bin Kleb ambaye kamati yake ilifanya usajili mzuri ulioongeza rekodi kwa kuipa ubingwa wa 23 wa Bara msimu uliopita na kuelekea kurudia jambo hilo tena katika dirisha hili.

"Tupo kwenye mazungumzo na mchezaji wa nje ya nchi na mambo yakiwa tayari tutaweka wazi kama ilivyokawaida yetu."

Hata hivyo, taarifa zilizozagaa ni kuwa Yanga ipo kwenye mbio za kumsajili mshambuliaji wa Uganda anayewaniwa pia na Simba, Moses Oloya anayecheza soka nchini Vietnam.

Yanga inaendelea kusajili mchezaji wa ziada wa kigeni baada ya shirikisho la soka, TFF, kuahirisha hadi msimu ujao kuanza kutumika kipengele cha Azimio la Bagamoyo la mwaka 2010 ambacho kinataka timu zisisajili zaidi ya wachezaji watatu wa kigeni.

Yanga imeshawasajili Haruna Niyonzima (Rwanda), Didier Kavumbagu (Burundi) na Mbuyu Twite (JK Kongo) kutoka nje ya nchi mpaka sasa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa