Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba bado yamng'ang'ania Juma Kaseja


Juma Kaseja
 
Uongozi wa klabu ya Simba umekanusha kumtosa kipa wao chaguo la kwanza Juma Kaseja na kusisitiza kuwa bado nahodha huyo wa timu ya taifa (Taifa Stars) bado anayo nafasi ya kupewa mkataba mpya wa kuendelea kuichezea timu hiyo katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara utakaonza Agosti 24.

Kaseja aliyejiunga na Simba mwaka 2002 akitokea Moro United ya Morogoro, anamaliza mkataba wake wa kuitumikia klabu hiyo Jumapili ya Juni 30 mwaka huu.

Akizungumza na gazeti hili, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema kwamba suala la Kaseja bado liko mikononi mwa viongozi wa klabu hiyo na maamuzi yoyote yanaweza kufanyika ndani ya mwisho wa wiki.

Mtawala alisema kwamba kiufundi, Kaseja anakubalika lakini nje ya uwanja ndiyo kuna maneno 'yanayommaliza' kipa huyo ambaye pia ni nahodha wa klabu yao.

"Kiufundi huwezi kumuacha Kaseja kirahisi. Lakini kuna mambo mengi yanazunguka katika usajili wake na hivyo ni lazima watu wakutane na kujadiliana kwa hoja kabla ya kufikia muafaka, ila bado kikao cha mwisho hakijafanyika na hivyo binafsi siwezi kusema kama atakuwapo au hatakuwapo msimu ujao," aliongeza Mtawala.

Alisema kwamba pamoja na lawama anazopewa kipa huyo na baadhi ya mashabiki, ukweli unabaki kwamba kwa ujumla wake, bado ni kipa hodari na amekuwa akikubali kuitumikia timu hata pale ambapo hakuwa ametarajia kuanza kutokana na sababu mbalimbali zinazojitokeza kwenye kikosi.

"Tofauti na timu nyingine makipa wengi wanadaiwa kutopendana, kwa Kaseja na Dhaira wao hiyo ilikuwa tofauti, wanashauriana na kuzungumza mara kwa mara," alisema Mtawala.

Simba ilimaliza msimu uliopita ikiwa katika nafasi ya tatu hivyo mwakani haitashiriki mashindano yoyote ya kimataifa.
Kocha wa klabu hiyo, Abdallah Kibaden 'King' aliumbia mtandao huu hili hivi karibuni kuwa si yeye aliyemtema Kaseja bali viongozi wa klabu hiyo ndiyo wanajua siri ya sababu ya kuliondoa jina la kipa huyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa