Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kamati ya ligi yaichimba mkwara Yanga

KAMATI ya ligi jana imeweka hadharani kuwa endapo mabingwa wa soka nchini Yanga watashindwa kuudhuria sherehe za utoaji zawadi za washindi ligi kuu ya Vodacom itakiona chamoto, Mwenyekiti wa kamati Wallace Karia amesema kuwa haoni sababu za Yanga kugomea zawadi hizo.


Sherehe za kukabidhi zawadi kwa washindi wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara zitafanyika Julai 3 na mgeni rasmi ni waziri wa habari michezo na utamaduni Mhe Fenella Mukangara, Yanga imetangaza kususia sherehe hizo za utoaji wa zawadi kwa madai ya kucheleweshwa.

Kupitia msemaji wake Baraka Kizuguto, Yanga imetangaza kutoudhuria katika utoaji wa zawadi hizo kwa madai ya kucheleweshewa zawadi zao ikiwemo fedha za ubingwa, Sababu za Yanga zimepingwa vikali na kamati ya ligi ambapo yenyewe imesema hata Yanga isipoudhuria sherehe hizo zitafanyika.

Karia amesisitiza kuwa Yanga ni kitu gani hata kama wamesusia ni bora wasusie na zawadi zenyewe, Ameongeza kuwa hawataibembeleza kwa lolote kwani wanaostahili kupewa zawadi si wao peke yao.

Yanga imemaliza kama mabingwa wa bara wakati Azam ikishika nafasi ya pili huku Simba ikikamata nafasi ya tatu, Kagera Sugar ilishika nafasi ya nne ambapo pia zinastahili kupata zawadi zao, Kama Yanga ikikataa itawanyima nafasi wachezaji wake ambao wengine wanastahuili kupewa zawadi ya uchezaji bora au mchezaji mwenye nidhamu

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa