Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HISPANIA WAING'OA ITALIA KWA MATUTA KOMBE LA MABARA, FAINALI NA BRAZIL MARACANA...NI BALAA

Close shave: Spain moved through to the Confederations Cup final after beating Italy on penalties in FortalezaHISPANIA imeitoa Italia katika Kombe la Mabara kwa ushindi wa matuta wa 7-6 mjini Fortaleza, kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 katika mchezo wa Nusu Fainali usiku huu.

Wataliano walifungwa na Waspanyola katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana, itawakutanisha wenyeji La Roja na Brazil wenyeji.
Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja ya penalti 14 na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na kuipeleka Hispania Fainali.


Dramatic: Spain triumphed 7-6 in a dramatic shootout to set up a dream final against Brazil
Ushindi wa mbinde: Hispania wakishangilia 7-6 na sasa watamenyana na Brazil
Heartbreak: Italy were left devastated after pushing the world and European champions the distance
Maumivu: Italia wameng'oka

Si zaidi ya mwaka uliopita, Italia walipigwa 4-0 mjini Kiev, lakini The Azzurri waliwasili Fortaleza wakiamini kisasi kinawezekana, ingawa haikuwa hivyo.
Mikwaju ya penalti;  Jesus Navas alifunga a ushindi na kufanya 7-6 , baada ya Leonardo Bonucci mkwaju wake kuota mbawa.
Wengine wote waliotangulia walifunga; upande wa Hispania ni Sergio Busquets,  Juan Manuel Mata,  Sergio Ramos, Gerard Pique, Andries Iniesta na Hernandez Xavi.
Italia ni Riccardo Montolivo, Andrea Pirlo, Sebastian Giovinco, Daniele De Rossi, Alberto Aquilani na Antonio Candreva.
Kikosi cha Hispania kilikuwa: Casillas, Arbeloa, Sergio Ramos, Pique, Jordi Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Pedro/Mata dk79, Torres/Javi Martinez dk94 na Silva/Jesus Navas dk52.
Italia: Buffon, Maggio, Bonucci, Barzagli/Montolivo dk45,Chiellini, Candreva, De Rossi, Pirlo, Marchisio/Aquilani dk79, Giaccherini na Gilardino/Giovinco dk91.
Off target: Italy blinked first in the shout-out when Leonardo Bonucci fired over at 6-6
Anakosaaa: Leonardo Bonucci mkwaju wake uliota mbawa
Decisive: Jesus Navas stepped up to score the winning penalty and send Spain to the final
Ya ushindi: Jesus Navas alifunga ya mwisho, chini anashangilia
Jesus Navas
Jesus Navas
Glamour: Worldwide superstar Shakira was in the stands in Fortaleza
Shakira alikuwapo jukwaani Fortaleza 
This one is for you: Pique celebrates Spain's victory by the tightest of margins
Hii ni kwa ajili yako: Pique akishangilia ushindi wa Hispania
Support: Shakira was watching her partner Pique in action for Spain 
Shakira jukwaani
Greetings: Shakira meets FIFA president Sepp Blatter in the VIP lounge
Shakira alikutana na Rais wa FIFA, Sepp Blatter katika eneo la VIP uwanjani
Support: Shakira was watching her partner Pique in action for Spain
Shakira akimuangalia mpenzi wake Pique akiichezea HispaniaOn the box: A spectator enjoys the party atmosphere in Fortaleza
Shabiki
Evens: The teams were locked at 0-0 after 120 minutes in the all European semi-final
Dakika 120 ziliisha 0-0 
Outnumbered: Italy's Giorgio Chiellini tries to win a header against Sergio Ramos and Gerard Pique
Giorgio Chiellini wa Italia akijaribu kupiga kichwa katikati ya Sergio Ramos na Gerard Pique
Effort: Fernando Torres attempts a shot on goal as Gianluigi Buffon watches
Jitihada: Fernando Torres alifumua shuti lililopanguliwa Gianluigi Buffon
Stretch: Christian Maggio gets his head to the ball in front of Spanish goalkeeper Iker Casillas
Anateleza: Christian Maggio alikaribia kumtungua kipa wa Hispania, Iker Casillas
On the ball: Manchester City's David Silva attempts one of his elusive runs
David Silva akipasua
Held his nerve: midfielder Andres Iniesta slotted his penalty past Buffon in the Italian goal
Andres Iniesta alimtungua Buffon kwa penalti

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa