Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CAVANI AWATOSA WAZAZI WAKE, AWAAMBIA WASIMFUATILIE MAISHA YAKE

Wanted man: Cavani is one of Europe's hottest propertiesMSHAMBULIAJI wa Napoli, Edinson Cavani amewapiga stop wazazi wake kuzungumzia mustakabali wake kwenye umma.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 wa Uruguay, alikuwa tayari amehusishwa na mpango wa kuhamia Manchester City, kabla ya mama yake kusema amefanya mazungumzo na klabu zote, City na Real Madrid.
Kisha maelezo ya baba yake yakapendekeza Cavani amekubali kujiunga na Real, kwa dau la Euro Milioni 63 (Pauni Milioni 54).
Hitting out: Cavani trains with his Uruguay team-mates in Brazil on Tuesday
Amewatolea uvivu: Cavani akifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa Uruguay nchini Brazil jana
Hitting out: Cavani trains with his Uruguay team-mates in Brazil on Tuesday
Lakini Cavani, ambaye amefunga mabao 29 katika ligi akiwa na Napoli msimu uliopita, amewataka wazazi wake wakae kimya na wakati ukifika utatoa majibu.
Akinukuliwa na La Repubblica, aliwaambia Waandishi wa Habari: "Baba yangu amezungumza kuhusu Real? Nataka niseme hayo maneno si yangu.
"Nimewaambia wazazi wangu mara elfu, wasizungumze tena. Wanaweza kuniumiza tu mimi.
"Mimi ni mali ya Napoli kama ilivyo na hiyo itategemea na klabu. Kama suluhisho lingine, litakuja lenyewe, tutamua.'
Rais wa Napoli, Aurelio De Laurentiis ameripotiwa akisema mshambuliaji wake huyo anatakiwa kufanya uamuzi juu ya mustakabali wake hadi kufikia Julai 20, akirejea kutoka kwenye Kombe la Mabara anakoiwakilisha Uruguay.
Na alipoulizwa ikiwa Real Madrid - ambayo sasa iko chini ya kocha wa zamani wa Chelsea na Paris Saint-Germain, Carlo Ancelotti - itakuwa sehemu yake sahihi, Cavani alibakia kuficha.
"Nitaweka wazi juu ya hilo pia - wakati wote nimekuwa nikisema ni moja ya klabu bora duniani.
Prolific: The Uruguayan was top scorer in Serie A last season
Anatisha: Nyota huyo wa Uruguay amekuwa mfungaji bora wa Serie A msimu uliopita
"Wote tumekuwa tukiota vizuri tu kuchezea timu yao, kama ambavyo tunaota kuhusu Barcelona, lakini sasa nipo Napoli na ninajivunia kwa kweli.
"Kama nitaiacha nyuma jezi ya bluu siku moja, nitajiunga na klabu kubwa tu. Wazi kuna mashabiki ambao wataelewa na wengine ambao hawataelewa.
"Lakini sitaki kuteleza nyuma ya mlango, Nataka kutoka mbele ya mlango, siku ambayo hatimaye mambo yatakuwa,"

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa