Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTANZANIA AZIDI KUTESA ULAYA

KIUNGO chipukizi Mtanzania, Adam Nditi jana aliendelea kuwa nje wakati timu yake, Chelsea ilipolala 1-0 mbele ya Norwich ugenini, bao pekee la Cameron McGeehan dakika ya mwisho kwa penalti katika Fainali ya kwanza ya Kombe la FA la Vijana.
Mechi ilionekana itaisha kwa sare hadi beki wa Chelsea, Alex Davey alipodaiwa na refa Neil Swarbrick kumuangusha kwenye eneo la hatari Joshua Murphy katika dakika ya pili ya dakika za nyongeza.
McGeehan hakuiangusha beji yake ya Unahodha na akaenda kuukiwamisha nyavuni mkwaju wa penalti akimtungua kipa Mitchell Beeney na kuwainia kwa shangwe mashabiki wa nyumbani, Uwanja wa Carrow Road ambao walikuwa zaidi ya 22,000. 
Chelsea ilitawala mchezo huo na kutengeneza nafasi nzuri, ambazo walishindwa kuzitumia, lakini waapewa nafasi kubwa ya kuupiku ushindi huo mwembamba katika mchezo wa marudiano nyumbani, Uwanja wa Stamford Bridge wiki ijayo.
Sasa ni mwezi wa pili, Nditi anayetokea visiwani Zanzibar anakosekana kabisa katika kikosi cha Chelsea, hata benchi hakai na haijulikani nini kinachomsibu kama ni majeruhi au amepokonywa namba.
Lakini BIN ZUBEIRY itaendelea kufuatilia ili kujua ukweli juu ya kiungo huyo aliyebeba matumaini ya Watanzania wengi kwamba ataling'arisha jina la nchi yake katika klabu kubwa Ulaya.
Kikosi cha Norwich City kilikuwa: Britt, Norman, Wyatt, McGeehan, McFadden, Toffolo, Murphy, Randall, Morris, King/Young na Murphy.
Chelsea: Beeney, Aina, Davey, Ake, Wright, Baker, Kiwomya, Loftus-Cheek, Feruz/Musonda, Colkett/Swift na Boga
Late: Norwich's Cameron McGeehan smashed home from the spot to give the Canaries a slender first-leg lead
La ushindi jioni: Nahodha wa Norwich, Cameron McGeehan akifunga kwa penalti. Chini anapongezwa na wenzake.
Norwich's Cameron McGeehan

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa