Simba yawaashia taa ya kijani Slavia Prague
SIMBA rasmi wamewajibu Mabingwa wa Jamhuri ya Czech, Slavia Praha kuwa wanawapa siku 14 tu za majaribio pamoja na vipimo vya afya kwa Beki wao Hussein Ally Mbegu na sio miezi mitatu kama ambavyo Praha walitaka hapo awali kwakuwa wana mipango nae kuelekea msimu mpya endapo majaribio hayatofanikiwa.
Praha wanaoshiriki UEFA Champions League wamekubaliana na masharti ya Simba na tayari Kijana na Menejiment yake wameanza mchakato wa VISA ili asafiri haraka iwezekanavyo kuelekea barani Ulaya.
