Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com
Simba yaanza na Kelvin Nashon
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
KLABU ya Simba SC imemtambulisha kiungo Kelvin Nashon Naftali kuwa mchezaji wake mpya kwanza kuelekea msimu ujao akijiunga na Wekundu hao wa Msimbazi kutoka Pamba Jiji FC ya Mwanza.
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Kocha mkuu wa Simba Steve Barker,amewambia viongozi wake kuwa january hii anahitaji wachezaji wapya watano. Steve Barker,anataka Left-back,Kiungo namba 8,kiungo namba 10,winga wa kulia na beki mmoja wa kati. Lakini pia kocha huyo amesisitiza kuwa wachezaji wawili kati ya hao watano watatoka South Africa (Kiungo namba 8 na winga).
Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa