MO Dewji uso kwa uso na wachezaji wapya Simba

Rais wa Simba SC, Mohammed Dewji amekutana na kufanya mazungumzo na wachezaji wapya watatu ambao tayari wametambulishwa Kelvin Nashon, Nathaniel Chilambo na Bakari Msimu.

Mo Dewji amewakaribisha wachezaji hao kwenye familia ya Simba na kuwaeleza malengo ya Simba ya ndani na kimataifa na hivyo kuwataka kujituma wakati wote wanapokuwa kwenye majukumu ya kuipambania nembo ya klabu.

Mwenyekiti wa Bodi, Crescentius Magori alikuwepo pia katika kikao hicho.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons