Yanga yaanza na Mwanengo

KLABU ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji chipukizi, Emmanuel Samuel Mwanengo (22) kuwa mchezaji wake mpya akijiunga na timu hiyo kutoka TRA United ya Tabora.

Mwanengo aliibukia Nyangobo FC ya Zanzibar kabla ya kwenda Tajikistan mwaka 2023 ambako alichezea Ravshan Kulob na Vakhsh mwaka 2024, kabla ya kurejea nchini mwaka huu kujiunga na TRA United, zamani Tabora United.

Na baada ya kuonyesha uwezo wake katika Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara ndani ya Nusu msimu anahamia kwa Wananchi kuendeleza kampeni ya kushinda mataji.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI