Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Boli la Stars limewatesa Nigeria mwanzo mwisho AFCON

Anaandika  Ephrahim Mabena

Dakika 30 za kipindi cha kwanza zilikuwa tamu sana Kuitazama Stars iliyojaa energy,Kasi na confidence ya juu sana ,Walizua vyema mno na walijaribu kukaa na mipira Kwa dakika kadhaa

Nigeria walipata Wakati Mgumu mno kuwafunga stars iliyokuwa na ujasiri mkubwa dakika zile 30 za mwanzo

Zuberi Foba ni Golikipa mzuri na ameonyesha MWANGA mzuri kwenye timu ya Taifa licha ya kufungwa lakini amepunguza Idadi ya magoli Height yake ilifanya saves nzuri mbele ya vichwa vya Osimhen na Ajay ambao Kwa kimo na warefu haswa.

Ibrahim Bacca Leo ameonyesha namna gani yeye ni sajenti kwenye Taifa,Victor Osimhen amekuwa na Wakati mwingi Mgumu mbele ya Bacca mpaka Kuna Wakati alikuwa Anataka huruma ya mwamuzi, Kiufupi Bacca Leo amekuwa Bora mno akiambatana na Bakari Mwamnyeto wamekuwa na utulivu sana eneo la ulinzi.

Victor Osimhen analala akiota jina la Sajenti Ibrahim Bacca,Kila alipotupa miguu na Bacca alikuwa nyuma yake , kiufupi Osimhen kawekwa mifukoni mwa sajenti Bacca Leo

Novatus Dismas Leo pasi nyingi alikuwa anapoteza kwenye eneo la kiungo

Ule mguu wa Kushoto wa Chukweze umejaa Sanaa kubwa sana ya kutembea na mpira, walinzi wa Stars waliteseka sana juu yake.

Nigeria wameshinda lakini furaha haipo ,Stars wamewapa mechi ngumu sana mastaa wa Nigeria

Kelvin John upewe nini pale kufunga tena dakika za jioooni zile

Mkeka wa mwanetu Davido wa Both team to score umetiki

Anyways tumefungwa ila furaha ya Vijana wetu kuwaona wakivuja jasho Bila uoga Wala papara

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa