Yanga yakabidhiwa milioni 10 za mama Samia
Katibu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa amekabidhi Sh. Milioni 10 kwa klabu Yanga, zawadi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya ushindi wa 2-0 leo dhidi ya Wiliete SC ya Angola katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.