Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YAIFANYIA UMAFIA MKUBWA YANGA, YAMPORA STRAIKA NA KUMWAGA WINO.

Katika kuhakikisha kikosi cha Simba kinarejesha makali yake kwenye msimu ujao wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, uongozi wa timu hiyo umefanikiwa kunasa saini ya mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars), Paul Kiongera.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini kutoka katika kamati ya usajili ya timu hiyo, Kiongera, ambaye ni mchezaji wa KCB inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka ya Kenya, amesaini mkataba wa miaka miwili.

Chanzo hicho kilisema kuwa kwa sasa Kiongera ni mmoja wa washambuliaji wanaoaminiwa na kocha mkuu wa Harambee Stars, Adel Amrouche na vile vile Kocha Mkuu wa Simba, Mcroatia Zdravko Logarusic, anatambua uwezo wake.


"Tayari wameshamalizana na Kiongera," kilisema chanzo chetu.Kiongozi huyo alisema mshambuliaji huyo anatarajiwa kuwasili nchini siku yoyote kuanzia keshokutwa ili kukamilisha taratibu nyingine za usajili.

Habari zaidi kutoka Simba zinaeleza kuwa bado mazungumzo na kiungo wa zamani wa timu hiyo, Jerry Santo, ambaye aliichezea Coastal Union hayajakamilika.

"Santo bao, kuna vitu wanaviangalia kwanza halafu watafikia maamuzi," aliongeza.Wakati huo huo, Logarusic anatarajiwa kurejea nchini leo jioni akitokea kwao Croatia ambako alikua likizo baada ya msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Bara kumalizika.

Mara baada ya kurejea nchini, Logarusic, anatarajiwa kukutana na uongozi mpya wa klabu hiyo ulioingia madarakani hivi karibuni kwa ajili ya kufanya mazungumzo na hatimaye kusaini mkataba mpya wa kukinoa kikosi cha Wekundu wa Msimbazi.

Logarusic ambaye alitua nchini mapema Desemba mwaka jana na kurithi mikoba ya Abdallah King Kibaden, alipewa mkataba mfupi wa miezi sita ambao ulimalizika Mei 31, mwaka huu.

Simba inatarajia kuondoka nchini Julai 20, mwaka huu kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya kuweka kambi maalumu ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi ambayo itaanza Agosti 24.

Kikosi hicho kinatarajiwa kuweka kambi ya siku 17 katika jiji la Johannesburg na mara baada ya kurejea itacheza mechi ya utambulisho wa kikosi chao itakayofanyika Agosti 8, mwaka huu katika tamasha maalum la 'Simba Day'.

Mbali na Simba, timu nyingine ambazo zinajiandaa na ligi hiyo ni pamoja na bingwa mtetezi Azam, Yanga, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar, Mbeya City, Prisons, JKT Ruvu, Ruvu Shooting, JKT Mgambo, Coastal Union, Ndanda FC, Stand United na Polisi Morogoro.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe