Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NIGERIA KUTETA NA STEPHEN KESHI

Shirikisho la kandanda la Nigeria NFF limesema kuwa linaanda mikakati ya kufanya mazungumzo na aliyekuwa kocha wa timu ya taifa Super Eagles Stephen Keshi wakimtaka aendelee kuhudumu kama mkufunzi mkuu. 


Kauli hii mpya ni tofauti na ile iliyochukuliwa na afisi iliyokuwepo awali ambayo ilikataa kuandikisha kandarasi upya naye.

Hata hivyo waziri wa michezo wa Nigeria anasemekana hakufurahishwa na matakwa mapya ya nyongeza ya mshahara alioitisha Keshi.

Keshi anasemekana kuwa aliomba kuongezewa mshahara wake maradufu hadi kutimia dola elfu thelathini ($30,000) kwa mwezi na kuwa pesa hizo zilipwe kabla hajaanza hatamu mpya.
Uongozi wake kocha Keshi umekumbwa na migomo ya mara kwa mara kuhusiana na malimbikizi ya marupurupu ya wachezaji na mishaharaa yao.

Keshi hata hivyo anakumbukwa kwa kuingoza The Super Eagles kunyanyua kombe la mabingwa barani Afrika mwaka wa 2013 mbali na kutimu raundi ya pili ya kombe la dunia la mwaka huu lililokamilika huko Brazil mapema mwezi huu.
Maigari Aminu amen'golewa madarakani Nigeria
Kamati kuu ya NFF hata hivyo imeagiza mazungumzo yaanze kwa niya ya kuandikisha upya kandarasi naye katika kipindi cha juma moja lijalo.

Wakati huohuo waziri wa michezo Tammy Danagogo amewaasa wadau wa kandanda nchini humo kuzika tofauti zao na kuimarisha viwango vya kandanda .

Danagogo alisema kuwa maafisa hawana budi kusitisha malumbano na vita vya kungangania uongozi kwa niya ya kujifaidisha .

Waziri aliyasema hayo muda mchache baada ya kamati kuu ya NFF kumn'goa mamlakani mwenyekiti wa shirikisho hilo

Aminu Maigari kwa madai ya ufujaji fedha za shirikisho.
Kamati hiyo ilichukua hatua hiyo takriban juma moja baada ya mapatano kati yao na shirikisho la soka duniani FIFA kumrejesha mamlakani baada ya mahakama moja kumng'oa uongozini.

Makamu wake , Chief Mike Okeke Umeh, ndiye atakayechukua hatamu kama kaimu mwenyekiti wa NFF hadi uchaguzi ujao utakaofanyika Agosti tarehe 26.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe