Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MBWANA SAMATTA, THOMAS ULIMWENGU WAWASILI DAR TAYARI KUIKABILI MAMBAZ

WASHAMBULIAJI tegemeo wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu wamewasili Dar es Salaam asubuhi ya leo kujiunga na timu hiyo kwa ajili ya mchezo wa kimataifa dhidi ya Msumbiji ‘Mambas’ mwishoni mwa wiki.

Washambuliaji hao wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) wote wamewasili wakiwa fiti tayari kwa mchezo huo wa kwanza wa Raundi ya Pili na ya mwisho kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Morocco.


Mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam, wachezaji hao walisema kwamba wanashukuru wameruhusiwa mapema kuja kujiunga na Stars kwa ajili ya mchezo huo wa Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

“Tunashukuru tumefika salama, tunashukuru kuruhusiwa mapema kuja kwa ajili ya mchezo huu muhimu kwa taifa letu, nasi tunawaahidi Watanzania kupigana kwa nguvu zetu zote kwa kushirikiana na wenzetu waliopo kambini Mbeya, ili kuitoa Msumbiji,”alisema Ulimwengu.

“Mimi nashukuru nimekuja  nikiwa fiti, kama utakumbuka katika mchezo uliopita dhidi ya Zimbabwe nilikuwa majeruhi sikucheza, ila sasa nipo tayari kulipigania taifa langu, naomba Watanzania wajitokeze kwa wingi Jumapili kuja kutupa sapoti,”alisema Samatta kwa upande wake.

Samatta na Ulimwengu waliotua na ndege ya shirika la Misri wakitokea Tunisia ambako TP Mazembe imepiga kambi kwa ajili ya mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika, walielekea hoteli ya Courtyard katikati ya Jiji baada ya kuwasili JNIA.

Kikosi cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kilichopiga kambi Tukuyu mkoani Mbeya, kinatarajiwa kurejea keshokutwa Dar es Salaam kwa maandalizi ya mwisho na Samatta na Ulimwengu wataungana na wenzao siku hiyo.

Kwa sasa wachezaji hao watakuwa wakifanya mazoezi peke yao Dar es Salaam hadi watakapoungana na wenzao Ijumaa kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezeshwa na refa Mahmoud Ashour kutoka Misri.

Mambas nao wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam Ijumaa wakati mechi ya marudiano itachezwa kati ya Agosti 1 na 3 mwaka huu nchini Msumbiji.

Chanzo Bin Zubeiry

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe