Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HISTORIA YA WAARABU -2

Inaandikwa na Fikiri Salum

Ilipoishia

Nabii Ismail hakuwa Mwarabu lakini baada ya kukaa hapo Makkah na kutifuka chemchem ya Zamzam, walikuja Waarabu wa Kiyemeni wa kabila la Qurhum na walipoona maji hapo waliomba kubakia hapo na ndipo Nabii Ismail akakulia kwenye kabila hilo na kujifunza Kiarabu na kuoa katika kabila hilo.

Endelea

MASKANI YA MWARABU YA ASILI

Waarabu kama tulivyoeleza hapo nyuma mwanzo walikuwa wakiishi Yemen lakini baadaye wakaanza kutawanyika kwenye sehemu nyinginezo za Bara Arabu, na Kwa kuwa wengi wao walikuwa wakiishi maisha ya kibedui ya kusafiri kutoka mahali pamoja kwenda kwingine kutafuta chakula na maji kwa nafsi zao na wanyama wao.

Waliweza kuenea sehemu zote za Bara Arabu na kufika Shamu na Iraq na Misri na Afrika mashariki na Afrika Kaskazini, kutawanyika huku kulizidi kwa kasi baada ya kuvunjika bwawa lao kubwa lililokuwa Maarib huko Yemen lililokuwa likilimbika maji mengi kwa ajili ya ukulima na mabustani yao na malisho ya wanyama wao.

Na mtawanyo mkubwa wa pili ni baada ya kuja Uislamu na kuhitaji kupeleka watu sehemu mbalimbali ulimwenguni kueneza dini hii.

Hapo ndipo Waarabu walipotawanyika kila mahali ulimwenguni kueneza neno la mwenyezi Mungu na kufikisha ujumbe wake, na ndiyo maana leo tunaona Waarabu katika bara na Manara ya ulimwengu.

ULIMWENGU WA WAARABU LEO

Waarabu leo wako kila mahali ulimwenguni, lakini kila ukikaribia kwenye kitovu cha dunia ambacho Kiko bara Arabu, Uarabu unazidi kudhihirika zaidi na lugha yao inazidi kuwa fasihi zaidi na hapa ndipo mila zao zinazidi kuifadhiwa na kutiliwa mkazo.

Aidha Waarabu wanaishi kwenye nchi zaidi ya ishirini za mashariki ya kati, ikiwemo bara Arabu na Shamu na Iraq na nchi za Ghuba ya Uajemi (Uarabu) na Afrika Kaskazini na mashariki, kuna ushirikiano katika jumuiya ya nchi za Kiarabu.

IDADI YA WAARABU LIMWENGUNI

Waarabu ulimwenguni wanahesabika kuwa idadi yao imefikia mia tatu milioni (180,000), ijapokuwa kuna idadi kubwa vile vile ya watu wa makabila mengine ambao wanaishi kwenye nchi za Kiarabu kama Mairani na Wahindi na Maarmani na Wayahudi, Mabarbari na Waafrika na Maburushi, Wakurdi na Waturuki na wengineo.

Kwa upande mwingine, kuna Waarabu wengi sana ambao wametawanyika katika nchi mbalimbali za dunia kwenye Manara yote ya ulimwengu...
INAENDELEA


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe