Mamelodi yamtaka Lucas kurudi klabuni

Klabu ya Mamelodi Sundowns  imempa taarifa kiungo mshambuliaji Lucas Ribeiro (27) kuwa arudi klabuni hapo ili kuwatumikia kuelekea msimu ujao wa 2026-27.

Lucas Ribeiro mpaka sasa yupo nyumbani kwao nchini Brazil  baada ya kuachana na Curtural Leonesa ya Spain na ashafanya makubaliano ya awali na Al Ittihad SC ya Libya ili kujiunga nao kwa msimu mpya kwa ushawishi wa kocha Rhulani Mokwena.

Lucas Ribeiro anasubiri maamuzi ya FIFA ili afanye maamuzi ya mwisho kama atarudi Mamelodi Sundowns au atasaini mkataba wa Al Ittihad SC baada ya Sundowns kushitaki kuwa Lucas Ribeiro alivunja mkataba kimakosa bila kufuata taratibu zote hadi kujiunga na Curtural Leonesa. 


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI