Azam FC yalamba matapishi yake kwa Kipre Junior

WINGA Muivory Coast, Kipré Tiagori Emmanuel Junior Zunon ‘Kipre Junior’ amejiunga tena na Azam FC akitokea MC Algiers ya Algeria.

“Tunayo furaha kuwataarifu kuwa tumemrejesha nyota wetu wa zamani, Zunon Kipre Emmanuel Junior, baada ya kumnunua kutoka klabu ya MCA | Mouloudia Club d'Alger. Welcome back home, Zunon Kipre Emmanuel Junior “ wameandika Azam FC kwenye page yao.

Kipre Junior anarejea Azam FC ambako awali alicheza kuanzia msimu wa 2022-2023 akitokea SOL FC d’Abobo ya kwao, Ivory Coast hadi 2024-2025 alipohamia MC Algiers.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI