16 wapitishwa kugombea Yanga
WANACHAMA 16 wamepitishwa kugombea nafasi za Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga kafika uchaguzi utakaofanyika Agosti 2, mwaka huu akiwemo Issa Ally Mangungu ambaye ni mdogo wa Mwenyekiti wa Simba, Murtaza Ally Mangungu.
Wengine waliopitishwa ni Hersi Ally Said anayetetea nafasi yake ya Urais na Arafat Haji anayetetea pia nafasi ya Makamu wa Rais na ambao wote hawana wapinzani.
