Diamond amuibua tena P Diddy
Nyota wa muziki wa kizazi kipya Afrika mashariki na aliyejipatia umaarufu mkubwa barani Afrika na dunia kwa ujumla, Nasseb Abdul "Diamond Platinums" ameamua kuwajibu Watanzania waliokuwa wanavumisha kwamba yeye amewahi kufanya ufuksa na msanii mkubwa Marekani na duniani kwa ujumla P Diddy. 'Nikweli nilienda kwa P diddy Tulikaa Studio na Tulikaa Hadi usiku na Tulienda hadi kwenye Swimming Pool, Tulimkuta Diddy akiwa na wasanii wake wa 2 wakike na wakiume, Ila kuhusu hayo mambo mengine nivile tu hii nchi watu wanapenda kuhusisha watu na vitu vyakipuuzi tu. Yaani mimi nifanyiwe ujinga Tambwe yaani Mimi Lama simba Dangote kweli?" Alisema Diamond kupitia Wasafi Fm.