Top scorer wa Simba Queens atimka
Mshambuliaji wa Simba Queens, Jetrix Shikangwa, ameondoka rasmi klabuni hapo na kujiunga na FC Masar ya Misri.
Jetrix anaondoka baada ya msimu bora, akifunga mabao 16 na kuwa mmoja wa nyota walioisaidia Simba Queens kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania.
Anatarajiwa kuungana na Mtanzania, Hasnath Ubamba, anayekipiga FC Masar.
