Ajitokeza kugombea na Injinia, Yanga
Mfanyabiashara mkubwa nchini katika sekta ya simu, Zahoro Matelephone, ameripotiwa kuchukua fomu katika makao makuu ya Klabu ya Yanga kwa ajili ya kuwania nafasi ya ujumbe kwenye uongozi wa klabu hiyo.
Hatua hiyo inaongeza ushindani katika mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa Yanga, huku wadau na mashabiki wakifuatilia kwa karibu majina yanayojitokeza kuwania nafasi mbalimbali.
Iwapo atafanikiwa kuchaguliwa, Zahoro atakuwa sehemu ya uongozi utakaosimamia maendeleo ya klabu kuelekea misimu ijayo.
