Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2026

Hans Raphael aamua kuwa shabiki wa Inno Loemba

UCHAMBUZI WA HANS RAPHAEL. . Kadiri muda unavyosonga nazidi kuwa shabiki wa Inno Loemba,to me huu ndo usajili bora wa Simba this January,jamaa ni Energetic pia amebarikiwa miguu mirefu ambayo inasapoti kwenye mikimbio yake…..jamaa anakimbia umbali mrefu sana,jamaa ana mapafu,jamaa anasafisha hadi hewa,muda wote anapanda na kushuka UP and Down. Nadhani akifanyia kazi umaliziaji wake basi ataimbwa sana

Simba yakataa uteja wa Yanga

WATANI wa Jadi, Simba na Yanga wametoshana nguvu kwa sare ya bila mabao katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya watani, Simba usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Kwa matokeo hayo, Yanga SC inafikisha pointi 29 katika mchezo wa 11 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi moja zaidi ya JKT Tanzania ambayo pia imecheza mechi sita zaidi. Kwa upande wao, Simba SC wanafikisha pointi 24 katika mchezo wa 11 pia, ingawa wanabaki nafasi ya tatu. Simba SC wameondoka uwanjani wakimlalamikia refa Msaidizi namba moja, Kassim Mpanga kukataa bao lililofungwa na mshambuliaji Suleiman Abdallah Mwalimu kipindi cha pili kwa kumhukumu alikuwa ameotea.

ATCL yasitisha safari za Dubai

Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limeufahamisha umma kwamba, kutokana na kufungwa kwa anga katika eneo la Mashariki ya Kati na kwa kuzingatia usalama wa abiria na wahudumu, safari zote za ndege kwenda na kutoka Dubai zimesitishwa hadi itakapotangazwa tena. Shirika hilo limesema linaendelea kufuatilia hali hiyo kwa karibu na kwamba safari zitarejeshwa mara tu hali itakapothibitishwa kuwa salama na tulivu. ATCL imewataarifu wateja wenye tiketi za kusafiri kwenda au kutoka Dubai katika kipindi hiki kuwa wanaweza kubadilisha safari zao bila gharama ya ziada, kulingana na upatikanaji wa nafasi. ATCL inaomba radhi kwa usumbufu wowote unaoweza kusababishwa na hali hiyo na inathamini uvumilivu na uelewa wa abiria wake katika kipindi hiki.

Yanga na Simba kutachimbika Zanzibar

Leo ndio leo katika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar pale watani wa jadi wa soka la Tanzania, Yanga na Simba watakaposhuka uwanjani kuwania pointi tatu muhimu mchezo wa Ligi Kuu bara. Yanga itakuwa mwenyeji ikiongozwa na kocha wake Pedro Goncalves raia wa Ureno wakati Simba inaongozwa na kocha wake Steve Barker raia wa Afrika Kusini. Tutegemee mchezo utakuwa mzuri na wa kuvutia, Yanga inataka kuendeleza rekodi yake ya kushinda mbele ya Simba wakati Simba nao wanataka kuhakikisha wanaondoa wimbi la kufungwa na Yanga na ikiwezekana wanapata ushindi ama sare.