Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limeufahamisha umma kwamba, kutokana na kufungwa kwa anga katika eneo la Mashariki ya Kati na kwa kuzingatia usalama wa abiria na wahudumu, safari zote za ndege kwenda na kutoka Dubai zimesitishwa hadi itakapotangazwa tena.
Shirika hilo limesema linaendelea kufuatilia hali hiyo kwa karibu na kwamba safari zitarejeshwa mara tu hali itakapothibitishwa kuwa salama na tulivu.
ATCL imewataarifu wateja wenye tiketi za kusafiri kwenda au kutoka Dubai katika kipindi hiki kuwa wanaweza kubadilisha safari zao bila gharama ya ziada, kulingana na upatikanaji wa nafasi.
ATCL inaomba radhi kwa usumbufu wowote unaoweza kusababishwa na hali hiyo na inathamini uvumilivu na uelewa wa abiria wake katika kipindi hiki.
