Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OZIL AITAMANI TUZO YA RONALDO

Kiungo wa klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ujerumani Mesut Ozil amesema miaka ijayo anaamini atashinda tuzo ya Ballon d’or na jinsi wachambuzi wanavyozidi kumkosoa ndiyo anapata nguvu ya kujituma zaidi.

Mjerumani huyo ameichezea Arsenal mechi 14 tu katika ligi kuu msimu huu kufuatia kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu akiuguza majeraha lakini tangu arudi tena uwanjani amekuwa katika kiwango bora.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa msimu uliopita akitokea Real Madrid anaonekana kuizoea ligi ya Uingereza tofauti na hapo awali. “Nikiendelea kufanya vizuri, afya yangu ikawa imara basi miaka michache ijayo Ballon d’or itakuwa mikononi mwangu” alisema Ozil. .”Ninajisikia vizuri. Mimi ni mchezaji mkubwa duniani,ninacheza katika klabu kubwa. Pia hii ligi tunatumia nguvu nyingi kuliko kule La Liga kwa hiyo ninazidi kuimarika zaidi kuliko mwanzo ” aliongeza Ozil.


Pia mchezaji huyo amesema kitendo cha kiungo wa zamani wa Manchester United Paul Scholes kuponda kiwango chake kilimuongezea nguvu ya kupambana na kuongeza kujituma zaidi.

Ozil sasa yupo katika majukumu ya timu ya taifa ya Ujerumani ambao jumapili watashuka dimbani kuwavaa Georgia katika mechi ya kutafuta tiketi ya kufuzu michuano ya mataifa Ulaya yatakayofanyika mwaka 2016 nchini Ufaransa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa