Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Fadlu kutimka Msimbazi

Machapisho ya hivi karibuni

Tabora United sasa ni TRA United SC

Klabu ya Ligi Kuu ya TABORA UNITED imeuzwa rasmi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na itajulikana kama TRA UNITED.  Timu itakuwa bado chini ya Manager wa TRA Mkoa wa Tabora mpaka mwezi Januari 2026 ambapo itahamia Dar es Salaam. Mameja na wamutimishi wa TRA mikoa ambayo timu itacheza Ligi Kuu wamehamasishwa kuiunga mkono timu kwa kuipa hamasa. Timu hii ni mahususi kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari.

Kocha Willete aihofia Yanga

Kocha mkuu wa timu ya Willete ya Angola ambao ni wapinzani wa Yanga, Bruno Ferry amesema wao wanatambua kuwa Yanga ni klabu kubwa hivyo watakabilisna nayo. ''Yanga ni timu kubwa Afrika, ni mtihani mgumu kwetu, lakini ni changamoto nzuri kwetu, na tuko tayari kuikabili”  '' Utakuwa ni mchezo mgumu kutokana na ubora wa Yanga ila tumejiandaa kikamilifu Kupambana nao.'' Maneno ya Kocha wa mkuu wa klabu ya Wiliete Benguela - Bruno Ferry.

Mashujaa, JKT hakuna mbabe

WENYEJI, Mashujaa wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. Mashujaa FC inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ilitangulia kwa bao la mshambuliaji wa zamani wa Kipanga ya Zanzibar, Mundhir Abdullah Vuai dakika ya 79 akimalizia kazi nzuri ya mshambuliaji mpya, Suleiman Salim Rashid ‘Bwenzi’ aliyesajiliwa kutoka Ken Gold ya Mbeya iliyoshuka daraja. Aliyeinusuru timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kupoteza mchezo wa leo ni mshambuliaji mpya, Paul Peter Kasunda aliyesajiliwa kutoka Dodoma Jiji kwa kuisawazishia dakika ya 87 akimalizia kazi nzuri ya beki Anuary Kilemile Junior.

Petro de Luanda kuisapoti Yanga dhidi ya Willete

Mwenyekiti wa Klabu ya Petro de Luanda ya Angola, Tomás Faria leo asubuhi amemtembelea Rais wa Klabu ya Young Africans SC na Mwenyekiti wa Umoja wa Vilabu Afrika, Eng. Hersi Said, kwenye kambi ya Klabu yetu hapa Luanda, Angola katika hoteli ya Protea.

Simba yaigomea CAF

Klabu ya Simba SC imeiandikia barua Shirikisho la Mpira Afrika (CAF) kuwa hakuna vurugu walizozifanya katika mchezo dhidi ya RS Berkane katika fainali ya CAFCC Simba SC inataka adhabu walizoanishiwa awali na CAF ziondolewe na CAF wamepokea barua hiyo na wanaifanyia kazi

Minziro aenda kuipandisha Ligi Kuu bara BigMan FC

Kocha Fred Felix Minziro amejiunga na Bigman FC kama mkuu wa klabu hiyo kuelekea msimu ujao wa NBC Championship 2025/26. Minziro alishawahi kuwa kocha wa Bigman FC msimu uliopita kabla ya kwenda kujiunga na Pamba Jiji Football Club na sasa amerejea tena.