Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Taifa Stars yapiga mtu huko 2-0

Machapisho ya hivi karibuni

Simba yabisha hodi tena kwa Miguel Gamondi

Klabu ya Simba SC inadaiwa kuingia kwenye mazungumzo ya awali na Kocha wa Singida Black Stars, Miguel Ángel Gamondi, kwa uwezekano wa kujiunga na klabu hiyo kama Kocha Mkuu baada ya kukamilika kwa majukumu ya AFCON. Kwa sasa, hakuna uthibitisho rasmi kutoka pande husika, huku maamuzi yakisubiri mchakato wa majadiliano na ratiba za majukumu ya kitaifa.

Morice Abraham ana mkataba wa miaka miwili Simba SC

Morice Abraham alikuwa miongoni mwa target za Yanga kwenye dirisha dogo kwa kuwa awali Morice alikuwa na mkataba wa miezi sita (6). Niliwahi kuongea hapa kuwa miongoni mwa vitu vigumu kwa Morice ni wasimamizi wake na miongoni ni Mbwana Ally Samatta jamaa amenyooka sana hana kona kona. Hawajaruhusu migongano mingi kwa mchezaji wao kumpotezea muda walikaa na Simba kujua mpango wa timu kwa mchezaji wao, Simba wakamtandika nyundo ya miaka miwili kuendelea kusalia hapo. Nathibitisha Morice ataendelea kusalia Simba kwa miaka mingine miwili mbele ikiwa mpaka atakapopata timu nje na Tanzania.

Sowah afungiwa mechi 5, Kante naye majanga

NYOTA wa Simba SC, kiungo Msenegal Alassane Maodo Kanté na mshambuliaji Mghana, Jonathan Sowah wamefungiwa mechi tano kila mmoja na kutozwa Faini ya Sh. Milioni 1 kila mchezaji kwa makosa ya kinidhamu kwenye mechi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Desemba 7 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Wakati Kante amepewa adhabu hiyo kwa kumpiga teke kwa makusudi kiungo wa Azam FC, Feisal Salum Abdallah – Sowah ameadhibiwa kwa kosa la kumpiga kiwiko kiungo mwingine wa Azam FC, Himid Mao Mkami katika mchezo ambao Azam FC iliibuka na ushindi wa 2-0, mabao ya mshambuliaji Mkongo, Jephte kitambala Bola dakika ya 81 na winga Iddi Suleiman Nado dakika ya 89. Wawili hao wameadhibiwa baada ya kukutwa na Hatia katika kikao cha Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) cha kupitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu siku za karibuni kilichofanyika Desemba 15 Jijini Dar es Salaam. Aidha, kikao hicho pia kimemuondoa refa wa mchezo huo Abdallah...

Alexander Dos Santos amtumia salama Balla Conte, Yanga

Kiungo wa Yanga, Moussa Balla Conte, ametumiwa salamu za nguvu na kocha wake wa zamani Alexander Dos Santos, akimtaka kupambana na kurejesha heshima yake ndani ya mabingwa hao. Santos, aliyewahi kumfundisha Conte akiwa CS Sfaxien, amesema kiungo huyo ana kipaji kikubwa na haipaswi kukata tamaa kwa kutopata nafasi ya kucheza. Anamtaka afanyie kazi maeneo ambayo wachezaji wenzake wanamzidi kisha aongeze mazoezi binafsi ili kurudi kwenye ubora wake. Ameeleza kuwa Conte ni kiungo wa kisasa mwenye uwezo wa kupiga pasi ndefu, kukaba kwa nguvu na kuiongoza timu, akisisitiza kuwa tatizo linaweza kuwa kujiamini tu. Santos: “Conte ni mchezaji mzuri, anaweza kurudi kwenye kiwango chake kama akijipanga na kuongeza kazi ya ziada.”

Mdaula Rede Cup 2025 yaanza rasmi

Michuano ya kumtafuta bingwa wa Rede Mdaula Cup 2025 imeanza kutimua vumbi katika Kijiji cha Mdaula kata ya Bwilingu Chalinze mkoani Pwani. Michuano hiyo ilianza rasmi jana kati ya Mtambani na Mwandu na leo 16/12/2025 Matuli na Mdaula Girls. Uwanja wa Matuli shuleni

Malale Hamsini aitosa KMC, atua KVZ

Kocha Malale Hamsiki amejiunga na klabu ya KVZ inayoshiriki ligikuu Zanzibar, mazungumzo yamefanyika, mkataba umesainiwa. Malale ameshaanza kusimamia mazoezi kilichobaki ni utambulisho rasmi na huwenda kesho akasimamia mchezo wake wa kwanza wa ligikuu Zanzibar akiwa na KVZ!