Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Sowah afungiwa mechi 5, Kante naye majanga

NYOTA wa Simba SC, kiungo Msenegal Alassane Maodo Kanté na mshambuliaji Mghana, Jonathan Sowah wamefungiwa mechi tano kila mmoja na kutozwa Faini ya Sh. Milioni 1 kila mchezaji kwa makosa ya kinidhamu kwenye mechi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Desemba 7 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Wakati Kante amepewa adhabu hiyo kwa kumpiga teke kwa makusudi kiungo wa Azam FC, Feisal Salum Abdallah – Sowah ameadhibiwa kwa kosa la kumpiga kiwiko kiungo mwingine wa Azam FC, Himid Mao Mkami katika mchezo ambao Azam FC iliibuka na ushindi wa 2-0, mabao ya mshambuliaji Mkongo, Jephte kitambala Bola dakika ya 81 na winga Iddi Suleiman Nado dakika ya 89.

Wawili hao wameadhibiwa baada ya kukutwa na Hatia katika kikao cha Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) cha kupitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu siku za karibuni kilichofanyika Desemba 15 Jijini Dar es Salaam.

Aidha, kikao hicho pia kimemuondoa refa wa mchezo huo Abdallah Mwinyimkuu kwenye orodha ya waamuzi wa Ligi Kuu kwa mizunguko mitano kwa kushindwa kuchukua sahihi dhidi ya wachezaji hao mara tu walipoyatenda.

Katika kikao hicho cha Bodi, kiungo Mganda wa Singida Black Stars, Khalid Aucho amefungiwa mechi tano pia na kutozwa faini ya Sh. Milioni 1 kwa kosa la kumsukuma mchezaji wa TRA United, Adam Adam, huku refa wa mchezo huo, Alex Pancras akipewa onyo kali kwa kosa hilo.

Kwa upande wao mabingwa watetezi, Yanga SC wametozwa Faini ya Sh. Milioni 5 kwa kosa la shabiki wake kuingia ndani ya Uwanja na kwenda lango la wapinzani, Coastal Union akionekana kama anatafuta au anaweka kitu kwenye mchezo mwingine wa Ligi Kuu Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...