TRA yaiua Namungo pale pale kwa Majaliwa

TIMU ya TRA United imetinga Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Namungo FC jioni ya leo Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.

Mabao yote ya TRA United inayofundishwa na Kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Mrundi Etienne Ndayiragijje yamefungwa na wachezaji wazawa, winga Denis Nkane na kiungo Ally Ng'azi.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons