Makonda amteua Leodgal Tenga kamati ya AFCON
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Christian Makonda amemteua Nahodha wa zamani wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Leodegar Chilla Tenga kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ndani ya Maandalizi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 ambazo Tanzania inaandaa kwa ushirikianona majirani, Kenya na Uganda.
