KLABU ya Yanga imeiandikia barua Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TBLB) kuomba ufafanuzi wa kina juu ya adhabu iliyotolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya TPLB, maarufu kama Kamati ya Saa 72 kwa mchezaji Suleiman Abdallah Mwalimu kufungiwa mechi tatu badala ya tano kama ilivyokuwa kwa wachezaji wengine watano waliofanya makosa kama kama yake.
Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam, Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Shaaban Kamwe amesema kwamba wanahitaji Bodi iweke bayana kuna upekee gani wa tukio la Mwalimu lililoifanya Kamati ya saa 72 kutumia kanuni tofauti ya 41:5(5.2) na wengine watano kutumika kanuni ya 41:21.
