Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NABII MUSA KIONGOZI WA WANAISRAEL UTUMWANI MISRI- 2

Inaandikwa na Fikiri Salum

Ilipoishia

SAFARI YA KWENDA NCHI YA AHADI

KUT 12:29-42 inasimulia Waisrael wote walivyokimbia Misri pamoja na mifugo yao waliposikia mayowe kutoka nyumba za majirani wao wote.

Endelea.

Katika safari yao wakaongozwa na Mungu kwa sura ya wingu mchana na ya moto usiku (KUT 13;17-22; Yoh 8;12): hivyo Mungu alionesha wazi kuwa hawaachi hata kidogo bali anawashughulikia kwa namna tofauti kadiri ya mahitaji.

KUT 14;5-31 inasimulia jinsi Wamisri, kisha kuwalilia wafu wao, walianza kuwatafuta Waisrael kwa Farao na magari wakawakuta karibu na bahari ya Shamu.

Lakini Waisrael walivuka bahari kama kwamba ni nchi kavu, kwa kuwa maji yamegawanyika, kumbe Wamisri wakazama kwa kuwa maji yamerudi mahari pake (EB 11;29) asubuhi Waisrael wakaona maiti za Wamisri wote zikielea, wakamshangilia Mungu aliyewaokoa.

(KUT 15:1-21 inatuletea wimbo ambao maneno yake ni kati ya yale ya kale zaidi katika biblia) , hivyo Mungu aliwaokoa tena watu wake katika maji na huu pia ni mfano wa ubatizo ambao unaadhimishwa hasa usiku wa Pasaka.

Hata katika hatari ya kukandamizwa Mungu alidai Waisrael watulie kwa imani ya kuwa ushindi ni wake tu, tena walitakiwa wasiyasahau kamwe mang' amuzi hayu, kwa kuwa ndiyo msingi wa imani ya dini yao.

Sisi vile vile tunatakiwa kukumbuka daima ubatizo wetu ambapo Mungu ameutoa, baada ya ushindi wa Pasaka safari ikaendelea mpaka kufikia nchi aliyoahidi Mungu, ila Waisrael wakaja kusahau uwezo wake na kumlalamikia kipumbavu hata kumchosha, KUT 10;1-11 inatuonya tusifanye vile.

Kama kawaida malalamiko ya kwanza yalihusu kula na kunywa (KUT 15;22-17-7) Mungu aliwakubalia kwa kuwaletelemshia Kwale halafu maana hasa chakula hicho kiliwashangaza Waisrael wakazidi kukikumbuka hata wakamdai Yesu awapatie tena kama kweli ndiye Musa mpya.

Yesu akawajibu kuwa mwenyewe ndiye chakula cha uzima kutoka mbinguni kinachotulisha safarini hapa (Yoh 6;23-59), vilevile kuhusu maji, Mungu alijitokeza katika mwamba huko Masa au Meriba, lakini alichukizwa sana na matendo (EB 3:15-19).

Shida nyingine ya kawaida kwa makabila ya wahamiaji ni kupigana vita Waisrael walilazimika kufanya hivyo na Waamaleki, wakapata ushindi si kwa nguvu zao, ila kutokana na sala ya Musa, mwombezi wao (KUT 17;8-16), sisi taifa la Mungu tunatakiwa tutegemee Sala kuliko uhodati wetu na daima tuwe na watu wenye kumwinulia Mungu mikono yao kama Musa Jangwani.

AGANO LA MLIMA SINAI

Walipofika mlima huo wa kutisha, Mungu alimuita Musa aupande Ili aseme naye, huku wengine wakibaki chini, hapo akampa Musa masharti ya agano lake na Waisrael (KUT 19) Akiwa muumba na hasa mkombozi wao alidai waishi kitakatifu kwa kushika amri kumi, ambazo tatu zinahusu heshima kwake na saba uhusiano na watu wengine (KUT 20;2-17)

Ndiyo mawe mawili ambayo Musa alipewa halafu Yesu akayakamilisha katika amri kuu ya upendo kwa Mungu na Kwa jirani (MK 12:28-34) amri hizo zinaweza kujulikana na kukubaliwa na mtu yeyote mwenye mapenzi mema.

Lakini Mungu alipenda kutusaidia tujue kwa urahisi na hakika zaidi tufanye nini Ili kumpendeza, tuwe watu wake naye awe Mungu wetu kweli kweli, Agano hilo upande wa Mungu ni imara kwa kuwa yeye ni mwaminifu kabisa, shida Iko upande wetu tulip geugeu, tukiahidi tusitekeleze, ndiyo sababu likahitajika agano lingine lililofungishwa na Yesu Kristo (2 Tim 2;11-13).

NDAMA WA DHAHABU

KUT 32 inatusimulia uasi wa Waisrael ulivyofikia kilele chake walipojitengezea Mungu wa dhahabu mwenye sura ya fahari (Biblia kwa dharau inasema "Ndama" na mla nyasi).

Hata Haruni alikubali kufuata matakwa yao huku mdogo wake akichelewa mlimani (Mdo 7;38-42) Israel kuabudu ndama ilikuwa chukizo mbele ya Mungu, kwa kuwa Mungu hana mbadala wa yeye kufanyiwa ibada.

INAENDELEA






Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe