Anaandika Musa Mwakisu
Nasreddine Nabi ndiye kocha aliyeleta mabadiliko makubwa ya uchezaji ndani ya klabu ya Yanga SC.
Haikuwa kazi rahisi kwake kwasababu wapo ambao walikuwa hawamuelewi na kuna muda kibarua chake kilikuwa kinashikiliwa na utandu wa buibui,ila imani yake juu ya filosofia yake ilimbeba sana.
Makocha wengi wamepita na kutengeneza filosofia zao kama babu Hans van der Pluijm,lakin mwalimu Nabi alikuja kuiamsha Yanga kwa njia zake.
Na kuitengenezea ubora mkubwa sana uwanjani,kila mchezaji anayeanza na anayekaa benchi wanakupa ubora ulele.
Zipo mechi nyingi sana ambazo Yanga SC walicheza kwa ubora na ujivuni wa hali ya juu kutokana na maarifa ya Nabi.
Leo nimesoma taarifa ya klabu ikisema kuwa kwenye tathimini yao ya michezo ya mzunguko wa kwanza,licha ya kufanya vizuri kwenye baadhi ya takwimu ila wamegundua kuna changamoto inayoifanya timu icheze soka tofauti na ile iliyozoeleka.
Ukiona mazingira kama hayo yanaelezwa kupitia barua rasmi ya klabu,bila shaka kuna shida kwenye benchi la ufundi kushindwa kuendana na filosofia ya klabu.
Mwalimu Nabi hana timu kwa sasa baada ya kuachana na Kaizer Chiefs,na ilisemwa wakati anaachana na timu hiyo ya Afrika ya Kusini aliamua kuwa karibu na mke wake aliyekuwa mgonjwa.
Bila ya kumvunjia heshima kocha Pedro Gonçalves hiki kilichoandikwa kwenye taarifa kwa umma,na kurejeshwa kwa Moalin inawezekana ikawa ni taa nyekundu au ya kijani.
Ila kilicho muhimu kama mambo hayatakwenda sawa,itakuwa ni wakati wa kufikiria kumrejesha baba wa filosofia ya Yanga SC kwa miaka ya hivi karibu kocha Nasreddine Nabi,ingawa cv ya kufundisha Afrika ya Kusini imempelekea kuwa kocha mwenye kuhitajika kulipwa pesa nyingi.
Bila shaka kwa bwanyenye GSM inaweza kuwa sio shida.
