Inaandikwa na Fikiri Salum
Ilipoishia
Mwa 22: 1-19 inatuletea habari ya kusisimua kuhusu sadaka ambayo Mungu alimdai Abraham yaani kumchinja Isaka, ni kimoja kati ya vielezo vya imani ya binadamu, imani inayooneshwa kwa matendo ya utiifu (Yak 2:21-22).
Endelea
Abraham hakusita kumrudishia Mungu kile alichopewa, akaondoka alfajiri akasafiri mpaka mahari alipoambiwa (Wayahudi) wanaamini mlima huo ndipo walipojenga hekalu la Yerusalem) kwa niaba ya waamini wote, Abraham alikuwa tayari kumchinjia Mungu mwanae pekee ampendaye.
Lakini kadiri ya Injili atakayemtoa kweli mwana pekee ni Mungu baba (Yoh 8-16) Yesu ndiye mwanakondoo aliyeuliziwa na Isaka na ambaye Mungu akajipatia juu ya mlima Kalivari alioupanda huku amejitwika kuni, basi mti wa msalaba.
Abraham aliamini uwezo wa Mungu juu ya mauti na hasa uaminifu wake kwa ahadi alizompa kwa hiyo akarudishiwa mwana hai kama mfano wa ufufuko, na katika yeye, yaani katika mzawa wake watu wote wakabarikiwa
Maisha ya imani yanadai daima sadaka, hasa ya mambo yanayopendwa zaidi (Rom 12:1-2) ndiyo njia ya kujaliwa baraka zinazopitia ubinadamu wetu.
Mwa 24 inasimulia kirefu jinsi Abraham kabla hajafa alivyomfanyia mpango wa ndoa Isaka kufuatana na mila zao, ila alikataa kabisa asirudi kwao, bali kwa vyovyote abaki katika nchi Ile aliyoahidiwa na Mungu.
Hivyo imani izidivkuongoza uzao wake kama ilivyomuongoza mwenyewe, Isaka akawa mrithi wa Abraham watoto 12 wa mwanaye Yakobo ni chanzo cha makabila 12 wa Israel hivyo Abraham huangaliwa pia kama Babu wa Wayahudi wote na Waarabu pia.
SALA YAKE (MWA 8:27)
"Nimeshika kusema na bwana Mimi ni mavumbi na majivu tu".
IBRAHIMU KATIKA KURANI
Hasa katika Uislamu Abraham (Ibrahimu) ni kielelezo muhimu cha imani kwenye Kurani hutajwa mara kwa mara katika sura 25 na mistari 245, kwa jumla habari zake zimekuwa tofauti na taarifa za biblia lakini heshima inalingana.
Habari zinazosimuliwa katika biblia juu ya Isaka babu wa Israel pengine hurudia kwenye Kurani na kutafsiriwa na wengi kuwa zilimuhusu Ismael kaka yake na babu wa Waarabu, anaaminiwa kuwa alijenga Kaaba kama msikiti.
MWISHO
Endelea kutazama Mambo Uwanjani Blog kesho kutakuwa na stori nyingine kali na ya kusisimua
