Inaandikwa na Fikiri Salum
DUNIA (kutoka neno la Kiarabu) wakati mwingine pia Ardhi na Kwa neno la asili la Kibantu nchi, ni Gimba la angani ambapo juu yake tunaishi sisi binadamu na viumbe hai wengine wengi, tukipata mahitaji yetu, kuanzia hewa ya kutufaa na maji.
Dunia ni mojawapo ya sayari zinazoelea katika anga la ulimwengu, kuna sayari nane zinazolizunguka jua, dunia yetu ikiwa sayari ya tatu katika mfumo wa juavna sayari zake.
Masafa baina yake na jua ni kilomita milioni 150 au kizio Astronomia 1, dunia huchukua siku 365, 256 kulizunguka jua, na masaa 23,9345 kuuzunguka mhimili wake na upana wake ni kilomita 12,756.
Dunia huwa na mwezi mmoja 1.
Umri wa dunia hukadiriwa kuwa na miaka bilioni 4,5 (1/2)
Ni mahari pekee katika ulimwengu panapojulikana kuna uhai ulioaminiwa kuanza miaka bilioni 3.5, hivi iliyopita, uhai unapatikana kwa spishi milioni 10-14 za viumbe hai pamoja na wanadamu waliokadiriwa kuwa sasa bilioni 7, 2 (4).
UMBO LA DUNIA
Umbo la dunia linafanana na tufe au mpira unaozunguka kwenye mhimili wake, mhimili wa dunia ni mstari kati ya nchi zake.
Lakini si tufe kamili, ina uvimbe kidogo kwenye sehemu ya ikweta, ilihali umbali kati ya ncha mbili ni kilomita 12,713 lakini umbali kati ya sehemu za kinyume ikweta ni km 12, 756.
Yaani kipenyo hivi kinazidi takribani kilomita 43 kipenyo kati ya ncha na ncha, tofauti hii inasababishwa na mzunguko wa dunia, kwani nje inasukuma sehemu za ikweta nje zaidi.
Kwa hiyo mahari duniani palipo karibu zaidi na anga la nje si mlima Everest kwenye Himalaya bali mlima Chimborazo nchini Ecuador (5).
Kwenye uso wake dunia huwa na tofauti kati ya nusutufe zake mbili nusu moja ina eneo kubwa la mabara yaani nchi kavu ambayo ni asilimia 47 ya sehemu hii.
Kinyume nusutufe nyingine inafunikwa na maji ya bahari na eneo la nchi kavu ni asilimia 11 pekee za maneno yake.
Kwa jumla dunia ni sayari pekee katika mfumo wa jua yenye maji katika hali ya Kiowevu usoni mwake, asilimia 96, 5 ya maji yote yaliyopo duniani, maji ya bahari huwa na asilimia 3, 5 chumvi ndani yake.
INAENDELEA
