Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kiungo Ghana, ahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kufanya ngono bila ridhaa

Kiungo wa kimataifa wa Nigeria na klabu ya Molde ya nchini Norway, Daniel Daga, ameingia kwenye msukosuko mkubwa wa kisheria baada ya kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela..

Hukumu hiyo imetolewa na Mahakama ya Wilaya ya Nordmøre na Romsdal nchini humo, kufuatia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 kupatikana na hatia ya kuhusika katika kitendo cha kingono bila ridhaa.

​Licha ya hukumu hiyo nzito, Daga pia ameamriwa kulipa faini ya Kroner 10,000 za Norway kwa ajili ya gharama za kesi.

Hata hivyo, mchezaji huyo kupitia mawakili wake amekata rufaa dhidi ya uamuzi huo, jambo linalomaanisha kuwa hukumu hiyo haitaanza kutumika mara moja mpaka pale mchakato wa rufaa utakapokamilika katika mfumo wa sheria wa Norway.

​Kufuatia sakata hilo, klabu yake ya Molde tayari imemsimamisha mchezaji huyo kushiriki mazoezi na shughuli zote za timu tangu tuhuma hizo zilipoibuka miezi miwili iliyopita.

Uongozi wa klabu hiyo umethibitisha kuwa Daga ataendelea kubaki nje ya kikosi wakati taratibu za kisheria zikiendelea, jambo ambalo linaweka rehani mustakabali wa kipaji hicho kilichowahi kung'ara na timu ya taifa ya Nigeria ya vijana (U-20) katika Kombe la Dunia.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe