Klabu ya Singida Black Stars imemfuta adhabu ya kusimamishwa kwa miezi mitatu mchezaji wake, Khalid Aucho, baada ya kupitia utetezi wake na kuomba radhi kwa makosa.
Uamuzi huu umefanywa na Kamati ya Nidhamu ya timu hiyo, kufuatia barua ya kukiri na kuomba radhi iliyotolewa na mchezaji huyo.
Aucho sasa anaruhusiwa kurejea kikosini na kuendelea kuitumikia timu hiyo.
Singida Black Stars inaendelea kusisitiza nidhamu, uwajibikaji na weledi kwa watumishi wake wote
