Inaandikwa na Fikiri Salum
Ilipoishia
Katika juhudi hizo Monasteri za Wabenedikto na Wamisionari waliotumwa katika Ulaya nzima walitoa mchango mkubwa, pamoja na ule wa Karolo mkuu, mfalme wa Wafaranki kabila la Kijerumanik muhimu zaidi katika historia, ambalo lilikuwa la kwanza kuingia kanisa katoliki moja kwa moja bila kupitia Ukristo na Kiario.
Endelea
KATOLO alitawazwa na Papa Leo 111 kuwa Kaisari wa magharibi (800), ushirikiano kati ya mapapa na makaisari wa Dola takatifu la Kiroma (Ujerumani wa leo na nchi kando kando) ulikuwa na mafanikio kadhaa na matatizo mengi zaidi na zaidi.
Baada ya Uislamu kuanza katika Karne ya 7 na kuteka maneno mengi ya Kikristo, kanisa katoliki liliona wajibu wake kuitikia maombi ya Wakristo waliohitaji msaada dhidi ya dhuluma iliyolenga kuwafanya wasilimu, ndiyo chanzo cha vita ya msalaba vilivyotawala karne zilizofuata.
Wengi wanaoma karne ya 13 kuwa kilele cha matunda ya kanisa katoliki katika kulea upya Ulaya magharibi kwa kuzaa hasa mashirikia ya ombaomba ya Fransisko wa Asizi na Dominikp Guzman, mitindo mipya ya sanaa, pamoja na vyuo vikuu walipostawi walimu wa kanisa kama Thoma wa Akwino na Bonaventura.
Utaifa uliotokea Ulaya magharibi kuanzia ufalme wa Ufaransa katika karne ya 14 ulivuruga umoja wa kanisa kiasi kwamba kwanza mapapa waliishi Avignan, mbali na Roma, kwa miaka 69 (1309-1378) halafu kwa miaka 38 (1378-1409) kukawa na farakano la kanisa la magharibi, waamini mengine waliomfuata Papa wa Roma na wengine Antipapa wa Avignon wakidhani ndiye Papa wa kweli.
Mambo hayo na makwazo mengine yaliwafanya wengi wadai bila mafanikio urekebishp wa kanisa tangu karne za nyuma, hatimaye yalichangia katika karne ya 16 ustawi wa matengenezo ya Kiprotestanti ambayo yalitenga na Papa sehemu kubwa ya Ulaya Kaskazini na kuvunjikavunjika katika madhehebu mengi.
Hapo juhudi za urekebisho wa Kikatoliki ziliongezeka na kuleta hali mpya hasa baada ya mtaguso wa Trento (1545-1563).
Kabla ya hapo, uvumbuzi wa njia za baharini za kufikia Amerika (1492), bara lililokuwa halijulikani na Wakristo, na Asia mashariki, ulichochea upya umisionari.
Kwa kuwa nchi zilizoshika kasi kwa kiasi kikubwa maneno mapya ya duniani kote wakati huo zilikuwa za Kikatoliki (Hispania na Ureno), kanisa kwa kutumia hasa mashirika ya kitawa uliweza kufidia upungufu uliosababishwa na Uprotestanti.
Upinzani dhidi yake uliojitokeza katika matengenezo hayo, ulizidi kupata nguvu katika zama za mwangaza ba mapinduzi ya Kifaransa (Karne ya 18) halafu katika ukoministi ulioenea kutoka Urusi hadi therusi moja ya dunia (Karne ya 20) na kuwa Wakatoliki milioni kadhaa (mbali na Waorhodoski wengi zaidi).
Mbele ya changamoto hizo mtaguso wa pili wa Vaticano (1962-1965) ulielekeza njia mpya za kuendeleza Ukristo katika ulimwengu wa kisasa.
Kwa mtazamo wa imani, historia hiyo yote inaonesha upande mmoja udhaifu na ukosefu wa Wakatoliki hata katika ngazi za juu, Mungu wa kuleta watakatifu wapya katika mazingira yoyote.
MWISHO
