Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KANISA KATOLIKI NA HISTORIA YAKE

Inaandikwa na Fikiri Salum

KANISA katoliki likiwa la zamani (Waorthodoksi) na Waorthodoksi wa mashariki wanashiriki sifa hiyo) na kubwa kuliko madhehebu yote ya Ukristo, historia yake inashika sehemu muhimu ya historia ya kanisa lote duniani tangu lilipoanza mwaka 30 hivi BK hadi leo.

Baada ya Yesu Kristo kuhubiri na kukusanya wafuasi kati ya Wayahudi wa Karne ya 1 hao walitumwa naye duniani kote, hasa wanaume 12 aliowaita mitume "yaani walitumwa". 

Waandamizi wao katika uongozi wa kanisa walianza kuitwa maaskofu, na kati ya yule wa Roma alizidi kushika nafasi ya pekee kwa sababu mtume Petro alifia dini katika mji huo kutokana na dhuluma dhidi ya Ukristo ambayo ilianzishwa na Kaisari Nero (mwaka 64) na kuendelea kwa kwikwi hadi ilipokomeshwa na Kaisari Konstantino mkuu aliyetangaza huko Milano Uhuru wa dini kwa wananchi wote (313).

Dhuluma haikufaulu kuzuia uenezi wa dini hiyo mpya katika Dola la Roma, mwishoni mwa  karne ya 2, maaskafu walianza kukusanyika katika sinadi Ili kuamua kuhusu masuala ya imani nk, mwaka 325 Konstantino aliitisha huko Nisea (Uturuki) mtaguso mkuu wa kwanza wa maaskafu wote Ili kurudisha umoja wa kanisa uliovurugwa na uzushi wa Ario kuhusu Yesu Kristo.

Mwaka 380 Kaisari Theodostus 1 alifanya Ukristo wa Kikatoliki kuwa dini rasmi ya Dola hilo kubwa lililoendelea kwa namna tofauti mashariki na magharibi kwa karne nyingi zilizofuata.

Ushindi huo ulifanya wengi watamani vyeo ndani ya kanisa, kwa kuwa viliendana sana na heshima na mali, hivyo ubora ulipungua, kabla yake Armenia ilikuwa nchi ya kwanza kupokea Ukristo kama dini ya taifa (301).

Ushindani kati ya majimbo makuu muhimu zaidi (Roma, Konstanhopoli, Aleksandria, Antiokio na Yerusalemu) ulisababidha mafarakano makuu (431,451,1054) yaliyoacha kanisa katoliki katika Ulaya magharibi karibu peke yake.

Huko, katika fujo iliyosababishwa na makabila yasiyostaaribika ya Wagermanik walioteka maneno yote ya magharibi, lilichukua jukumu la kuokoa ustaarabu wa Ugiriki wa kale na Roma ya kale uliokwisha athiriwa na Ukristo kwa kiasi kikubwa.

Katika juhudi hizo, Monasteri za Wabenedikto na Wamisionari waliotumwa katika Ulaya nzima walitoa mchango mkubwa, mfalme wa Wafaranki, kabila la Kijerumanik muhimu zaidi katika historia, ambayo lilikuwa la kwanza kuingia kanisa katoliki moja kwa moja bila kupitia Ukristo wa Kiario.

INAENDELEA

moja kati ya kanisa katoliki

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe