Iran inafikiria kujiondoa kwenye kombe la Dunia la 2026 huko USA, Canada na Mexico. Kulingana na chapisho la mamlaka la Marca, nchi haijafurahishwa na hali ya wasiwasi inayoongezeka baada ya shambulio la jana la kijeshi na Marekani na Israel.
Iran ilifuzu mwezi Machi mwaka uliopita kwa kuongoza Kundi A katika mchujo wa Asia, na hivyo kujihakikishia nafasi ya kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya saba.
Wamepangwa Kundi G pamoja na Ubelgiji, Misri na New Zealand, huku mechi zao zote zikiwa kwenye ardhi ya Marekani.
