Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HISTORIA YA MTUME MUHAMMAD NA UISLAMU- 4

Inaandikwa na Fikiri Salum

ILIPOISHIA

MTUME akamjibu "mimi sijui kusoma kwani sijapata kujifunza", akaja akamkamata, akambana akamwambia tena "soma", mtume akamjibu jawabu lile lile, hata mara ya tatu akamwambia "soma" iqra a bismi ra bbik.

Endelea.

Akamsomea sura ya 96 mpaka kati yake kisha mtume akaisoma kama alivyosomewa, hii ndiyo sura ya kwanza kushika katika kurani, ingawa haijawekwa mwanzo.

Mara yule mtu (malaika) akaondoka mwchoni pake asimwone, kaenda wapi, naye akarejea kwake hofu imemshika.

Alipofika nyumbani Khadija alidhani ana homa, akamfunika nguo gubigubi akakaa mbele yake akimsikiliza anavyoweweseka, homa ilipomwachia alimweleza Khadija yote yaliyomtokea, naye akamtuliza moyo wake, akamyakinishia ya kuwa hapana lolote baya litakalomzukia.

Mara bibi huyu akaondoka, akaenda kwa jamaa yake Waraga bin Naufat akampa habari yote iliyompata mumewe, naye akamwamrisha amwite na mtume akaenda akamweleza habari yake yote.

Bwana Waraga akamwambia "huyo ndiye Jibril, aliyemshukis Nabii Musa na Nabii Isa, basi jibashirie kuwa wewe ni mtume wa umma huu! Nami natamani kuwa hai nikuone unavyosimama kuwatengeneza jamaa zako, inshallah nitakuwa mkono wako wa kulia.

Wakarejea kwao hofu yote imemtoka baada ya kuazimia kuwa hatakwenda tena kule pangoni, palepale akaondoka akaenda pangoni mwake Ili aonane na makike tena, ingawa alikaa huko muda mrefu.

Siku Ile ya kupata utume inafikia mwezi Disemba 610, huyu Waraga hakuwa akiabudu dini ya sanamu bali alikuwa Mkristo, alipokuwa akisoma vitabu aliona kutatokea mtume mwingine, ndiyo maana alipohadithiwa habari Ile mara moja akaamini kuwa aliyemjia mtume ni Jibril.

MAISHA YAKE MAKKAH

Muhammad aliishi Makkah kwa miaka 53, arobaini (40) katika hiyo akiwa ni mtu wa kawaida kabla ya kupewa utume, na 13 akiwa ni mjumbe wa mwenyezi Mungu.

Maisha yake Makkah yalikuwa ya taabu utotoni mwake, kwani alizaliwa yatima kisha alipokuwa katika ujana wake alikuwa akifanya kazi ya kuchunga mbuzi na kondoo na watu wa Makkah kwa vijipesa kidogo mpaka alipofika umri wa miaka 25 akapata kazi ya kumfanyia biashara Khadija, bibi mtukufu wa Kikureshi ambaye baadaye alikuja kuwa mkewe na kuzaa naye aghlabu ya watoto wake.

MIAKA 13 YA UTUME MAKKAH

Katika miaka 13 aliyoishi hapo Makkah baada ya kupewa utume, Muhammad alipata kila aina ya mateso na masumbuko, juu ya nafsi yake na juu ya wafuasi wake, naye alisubiri na kustahimili kila aina ya taabu na shida kwa ajili ya mola wake, mpaka mwenyezi Mungu alipompa amri ya kuhama mji huo na kuelekea Madina.

Katika muda huo alipokuwa Makkah wengi wa jamaa zake na watu wengine wakubwa wa matabaka mbalimbali za jamii waliingia dini yake.

Mwaka 622 Wakureshi wakiona hasara katika mafungamano yao na Waarabu wengi wenye kuabudu miungu mingi kwa dukuduku zao zilimfanya Muhammad ahamie pamoja na sahibu wake Abubakar Assiddiq na wafuasi wake 70 hivi akaishi Yaithrib, mji ambao ulikaliwa na Waarabu na Wayahudi pamoja na ambao baadaye ukaitwa Madinat Al Nabi, yaani mji wa Nabii kifupi kifupi Madina.

Mwaka huo ukawa wa kwanza katika kalenda ya Kiislamu inayotumika tangu wakati wa Halifa Omar bin Khatab hadi leo.

KUHAMIA MADINA NA MWANZO WA UMMA

Mtume Muhammad baada ya kupewa amri ya kuudhuria Madina aliondoka na kuhama mji huo ambao ulimpokea na kumkubali na kumsaidia na kuntukuza na kumlinda na maadui.

Ingawa Wayahudi wa Madina walikataa kumsadiki kuwa nabii, kama wale wa Biblia, aliendelea kuhubiri huko na tangu mwaka wa kwanza alitunga hati ya Agano iliyokubaliwa na Wamadina wote ndiyo asili ya umma, jamii ya waumini.
INAENDELEA




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe