Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HISTORIA YA MTUME MUHAMMAD NA UISLAMU-2

Inaandikwa na Fikiri Salum

Ilipoishia jana.

KITENDO chenyewe alichokiazimia kuifanya mara mbili zote hizo na mwenyezi Mungu akamfadhi nacho ni kutaka kukesha katika ngoma za Arusi mbili za marafiki zake waliooa katika mji wa Makkah.

Endelea.

Lakini Mungu alimpa usingizi mkubwa katika masiku yote hayo mawili hata hakuweza kufumbua jicho, wala kunyanyua miguu kwenda mahari, hajapata kuudhuria hata mara moja katika ibada za kuabudu sanamu wala kula chakula kilichochinjwa kwa ajili yao, moyo wake ulichukizwa na hayo na mambo mengine yaliyo mabaya.

Tangu udogo wake mtume alipndokea na sifa nzuri ambazo hapana hata mtu mmoja katika hirimu zake aliyekuwa nazo zote, kila sifa zinazohesabiwa kuwa ni njema na ndizo alizokuwa nazo tangu utoto wake.

Mkewe Aisha alipoombwa kutaja kidogo sifa za mtume, alisema hivi, "sifa zake ni zile sifa nzuri zinazosofiwa na kurani na katika kurani zimetajwa chungu ya sifa zilizo nzuri.

Mtume mara nyingi alikuwa akisema sikupata kufanya hata siku moja yale mambo waliyokuwa wakiyafanya makafiri", kwa hivyo yeye hakupata kuabudu sanamu, kulewa, kuzini, kucheza kamari wala hakumdhurumu mtu kitu chake na kama haya.

Lakini alikuwa msemakweli, mwaminifu, mpole na mwenye haya na sifa nyingi nyinginezo bora kama hizi, watu wa Makkah walikuwa wakimsifu kwa tabia zake, hata wakampa jina la Muhammad Al Amin (mwaminifu) alikuwa hatajikani ila kwa jina la Al Amin.

Wakubwa na wadogo walikuwa wakimheshimu na kumpa amana zao kuwawekea, hata baada ya utume.

KABLA YA KUPEWA UTUME

Makureshi ni watu wa biashara, kila kureshi alipata kufanya kazi hii. safari moja baadhi yao walipokuwa wakienda Yemen katika biashara zao, baba yake mdogo wa pili bwana Zubeyr alimshauri ikiwa atapenda kusafiri, mtume aliridhia akaenda naye mpaka Yemen, wakakaa huko muda wa siku tatu tu kisha wakarejea, wakati huo mtume alikuwa mtoto wa miaka 9.

Hata alipotimia miaka 12 mwaka 582, alisafiri tena pamoja na baba yake mdogo mwingine, bwana Abu Talib.
 INAENDELEA





Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe