Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ally Kamwe afunguka makubwa Simba kufanya ushirikina, adai goli ni offside

Afisa Habari wa Young Africans, Ally Kamwe, ametoa malalamiko mazito dhidi ya wapinzani wao Simba SC, akidai kuwa mambo mengi yasiyo ya michezo yalitawala kuelekea kupatikana kwa sare ya 0-0 katika dabi iliyopita. Kamwe amedai kuwa kulikuwa na matukio ya utata ya uamuzi pamoja na vitendo vya ushirikina ambavyo viliisaidia Simba kupata alama hiyo moja.

​Katika andiko lake, Ally Kamwe amefunguka yafuatayo:

​"Kwanza ilikuwa OFFSIDE.. Pili, AKASHIKA. Move ikaruhusiwa kuendelea kama hakijatokea kitu. Sitaki kabisa kukumbusha kuwa Mchezaji huyu alitakiwa kufungiwa MECHI 5 kwa kosa la kumpiga kiwiko mchezaji wa Dodoma Jiji ... Sitaki kuwakumbusha, kuwa Waamuzi walishatishiwa kufungiwa Maisha kimpira na kupelekwa JELA kuhusu mechi hii.

​Turidi uwanjani, Watu hawa baada ya mazoezi ya mwisho siku moja kabla ya mchezo, wakagoma kuondoka uwanjani Usiku.. Wakafanya Ushirikina na vurugu za kila aina.. Wakaja kutolewa kwa msaada wa Polisi.

​Hawakumaliza, Siku ya mechi wametumia mlango wa VVIP kuingia uwanjani. Wakavunja mlango wa chumba cha Waandishi wa Habari. Muda wa Pitch Feeling, wakautumia kuzunguka uwanja na kufanya vitendo vya Kishirikina bila wasiwasi wote.

​Hapa Najaribu kuwaonyesha kwa uchache tu NGUVU iliyotumika hadi Makolo wamepata POINTI 1 kwenye Derby. Kimsingi, kwa mtu anayejua Mpira vizuri atakubaliana na mimi.. JANA SIMBA wamethibitisha ni WADOGO SANA KWA YANGA na watatumia miaka mingi sana kuja kushinda Derby.

​Nguvu yote kubwa sana Ilitumika ndani na nje ya uwanja haijaweza kufuta Uteja wao. Wana kikosi chenye wachezaji machachari na Viongozi wenye mihemko. Kama isingekuwa mambo ya kupelekana JELA, ikapigwa FAIR, Prince Dube angewaveka ile chuma ndio mngeona mengi zaidi jana...
​Wanazuga Kulalamika na kutukana watu leo ili kuficha Vitu vya hovyo walivyofanya na Wameshindwa kupata Ushindi .. Hii inawauma sana. KULIWA MARA 6 Imebaki pale pale na POINTI 5 ZIMESIMAMA VILEVILE." Ameandika Ali Kamwe. msemaji wa Yanga SC.

Ally Kamwe

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe