Klabu ya Al Ahly imetoa taarifa rasmi kufuatia kikao cha dharura kati ya Rais wa klabu, Mahmoud El Khatib, na viongozi waandamizi baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu.
Katika taarifa hiyo, klabu inakiri na kuelewa kusononeka na hasira za mashabiki kutokana na matokeo mabaya, huku uongozi ukichukua dhima kamili kwa yale yanayotokea.
Uongozi umekiri kuwepo kwa makosa ya kiufundi na kiutawala, ukiahidi kuwa hatua madhubuti za kurekebisha hali hiyo zinaandaliwa na zitahitaji muda kiasi ili kuleta tija.
Tayari maamuzi kadhaa ya dharura yamefanyika na yatatangazwa hivi karibuni, huku tathmini ya kina na mabadiliko ya kimfumo ndani ya idara ya mpira wa miguu yakianza kufanyiwa kazi ili kuendana na hadhi ya klabu.
Mwisho, uongozi umewashukuru mashabiki kwa uaminifu wao na kuahidi kufanya kila liwezekanalo kurudisha timu katika mstari uliozoeleka.
Maana ya Taarifa hii kuwa tayari kuna watu washaliwa vichwa ...Faini zimetembea na wenye kuajibishwa wamewajibishwa
